Na Fabius Clavery- Misalaba Blog, Kagera
Halmashauri ya wilaya ya misenyi mkoani Kagera inafanya jitihada za
kukagua na kuondoa masalia ya vifaa vya kivita
katika kata ya Nsunga iliyopo wilayani humo kufuatia kulipotiwa kwa uwepo wa
mabomu mara kwa mara katika kata hiyo ili kuwahakikishia usalama wakazi wa eneo
hilo.
Hayo yalielezwa na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilayani
humo ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo kanali Willison Sakullo wakati
akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani
cha halmashauri ya wilaya hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa
halmashauri mnamo october 28 mwaka huu .
Kanali Sakulo alikiambia kikao hicho kuwa tayari taratibu za
kuwasiliana na wahusika kutoka vikosi vya jeshi zinaendelea kufanyika ambapo
tayari halmashauri hiyo imekwisha andika barua kwenda kwa mkuu wa mkoa wa Kageraili kuwezesha zoezi
hilo.
"Ni kweli hili swala lilikwisha fika kwangu,na sisi kwa uzito
wake tumeliandikia kwenda kwa mkuu wa mkoa ili liandikiwe kwenda makao makuu ya
jeshi kuona kwamba wale wataalamu wanao husika na medani waje basi kufanya
angalau upekuzi katika lile eneo maana naambiwa kuna maandaki pale yaliachachwa
kipindi cha Idiamin vita ya Kagera,ni kama mara mbili tatu zimetokea taarifa
limekutwa bomu sasa tusingependa wananachi wetu waendelee kudhulika"
alisema Kanali Sakulo.
Kwa upande mwengine mkuu huyo
wa wilaya ametoa rai kwa madiwani kufuatilia ujenzi wa vyumba kumi vya madarasa
vinavyojengwa katika kata za halmashauri hiyo ambazo ni kata za Kashenye,
Buyango Bugandika Kilimilile Gabulanga Minziro Kakunyu na Kyaka ambapo
vinajengwa vyumba viwili.
"mweshimiwa mwenyekiti nawaomba waheshimiwa madiwani wafuatilie
pia katika huu ujenzi wa madarasa kumi yanayojengwa kama tulivyokuwa tunafanya
kipindi kile cha fedha za uviko 19ili madarasa haya yamalizike mapema mimi
wakati wa uzinduzi wangu kutokana na maelekezo ya mkuu wa mkoa nilitoa siku 35
ambazo zinaisha tarehe 25 mwezi wa 11, kwaio naomba tufatilie ili yamalizike
haraka" aliongeza Kanali Sakulo.
Mkuu huyo wa wilaya amesema Serikali ya jamhuri ya muungano wa
Tanzania inafanya hivyo ili kuhakikisha janauari madarasa yanakuwepo ya
kutosha.
Kadhalika mkuu huyo wa wilaya ametoa rai kwa madiwani wa kata zote za
wilaya hiyo kushughulikia masuala ya upungufu wa matundu ya vyoo katika shule
za msingi na sekondari za wilaya hiyo kwa kutoa hamasa kwa wananchi kwani
changamoto hiyo ni kubwa sana.
Post a Comment