" WAFANYABIASHARA NA WANANCHI MNADA WA SEKE MKOANI SHINYANGA WAMEITAKA SERIKALI KUWAJENGEA VYOO ILI KUZUIA ATHARI

WAFANYABIASHARA NA WANANCHI MNADA WA SEKE MKOANI SHINYANGA WAMEITAKA SERIKALI KUWAJENGEA VYOO ILI KUZUIA ATHARI

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Wafanyabiashara na wananchi wengine wanaotumia mnada wa Seke uliopo katika kata ya SekeBugoro Wilayani kishapu Mkoani Shinyanga, wameitaka Halmashauri hiyo kujenga vyoo katika eneo hilo, kama hatua ya kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya mlipuko.

Wameiambia Misalaba Blog kuwa kukosekana kwa huduma ya choo katika mnada huo inaweza kuchangia magonjwa ya mlipuko kutokana na watu wanaofanya shughuli katika eneo hilo kujisaidia ovyo.

Wameiomba halmashauri hiyo kutatua changamoto hiyo kama hatua ya ya kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya mlipuko, kwani tangu kuanza kwa mnada huo Mwaka 1984  hakuna huduma ya choo katika eneo  hilo.

Wamesema wamekuwa wakijisaidia ovyo hali inayotishia usalama wa afya zao,  na kwamba licha ya kuwasilisha changamoto hiyo kwenye mamlaka husika lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara Halmashauri ya Kishapu Dotto Yahaya amekiri kuwepo kwa  changamoto hiyo  katika mnada wa Seke ambapo ameeleza kuwa changamoto hiyo wamekuwa wakiiwasirisha kwa viongozi mbalimbali akiwa mtendaji wa kata, afisa biashara wa Halmashauri hiyo ambao wote hawakutekeleza ahadi zao.

“Hili jambo nimelifuatilia sana alikuja mtendaji wa kata tukamwambia afisa biashara wa Wilaya ya Kishapu bado ananipa ahadi lakini utekelezaji wake na ushirikiano tu kwetu haupo kwahiyo tunaomba serikali ngazi ya juu kama ni mkuu wa Mkoa wa Shinyanga atusaidie tusije tukafika huko tunakoelekea”.

 “Athari nyingi tu huwa zinatokea mimi nashuhudia watu wengi wanasumbuliwa na tumbo kwa sababu ya utumiaji wa maji ya kwenye madimbwi ya maji yanayozunguka mnada huu, watu huwa wanajisaidia haja zao hovyo  kwenye vichaka”.amesema Mwenyekiti Yahaya

 Naye katibu wa wafanyabiashara David Liwa ameeleza umuhimu wa vyoo katika mrada huo wa Seke uliopo Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga.

“Swala la choo tuliwaita wakaja tukaongea nao viongozi kutoka Halmashauri lakini mpaka sasa hawatekelezi sisi tumechoka kujisaidia ovyo kama wanyama, sisi bado hatujagoma kutoa ushuru lakini tunawapa muda tena endapo wakishindwa sisi tutafanya maandamano ya amani kudai haki zetu maana kipindi cha nyuma tulitaka kufanya mgomo wa kutoa ushuru  wakatuambia tukigoma wanakuja kufunga mnada huu”.amesema Liwa

Mnada wa Seke uliopo kijiji cha Ididi kata ya Bugoro Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga ambao pia unajumuisha Gulio la wiki unakadiriwa kuwa na takribani watu Mia tano na kwamba hakuna vyoo katika eneo hilo hali inayoendelea kuathiri afya kwa wafanyabishara na wananchi kwa ujumla.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara Halmashauri ya Kishapu Dotto Yahaya akielezea changamoto katika mnada huo.katibu wa wafanyabiashara David Liwa akielezea changamoto zilizopo katika mnada huo. 





Post a Comment

Previous Post Next Post