" VITU NA VIELELEZO VYA WIZI VYA KAMATWA SHINYANGA, JESHI LA POLISI TUMEJIPANGA KIKAMILIFU - KAMANDAMAGOMI

VITU NA VIELELEZO VYA WIZI VYA KAMATWA SHINYANGA, JESHI LA POLISI TUMEJIPANGA KIKAMILIFU - KAMANDAMAGOMI


Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishna msaidizi wa Polisi Janeth Magomi ameendelea kuwasihi wananchi kuacha vitendo vya uhalifu na kwamba wanapaswa kushirikiana na jeshi hilo katika kutokomeza uhalifu.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati  akitoa taarifa  ya misako na doria zilizofanywa na jeshi hilo katika  kipindi cha mwezi mmoja kuanzia Disemba 20, 2022 hadi Januari 23,2023 amewasisitiza wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kushirikiana na jeshi hilo ili kutokomeza uhalifu.

Kamanda Magomi amewataka wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi kwa kuwaadhibu wahalifu badala ya kuwafikisha katika vituo vya Polisi kwani kitendo hicho ni kosa la jinai na kinahatarisha usalama wa raia.

Amesema jeshi hilo  limefanikiwa kuwakamata watu 10 wanaotuhumiwa kujihusisha na  vitendo vya uhalifu ikiwemo wizi wa vifaa mbalimbali vya ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR kipande cha nne Tabora-Isaka na tayari wameshafikishwa mahakamani.

Ameeleza kuwa jeshi hilo limejipanga kikamilifu kuhakikisha linadhibiti mianya yote ya vitendo vya wizi katika mradi huo, ambapo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watu watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo.

Wakati huo huo Kamanda Magomi ametaja vitu na vielelezo mbalimbali vya wizi vilivyokamatwa kwa kipindi cha Mwezi mmoja kupitia doria na misako hiyo ikiwemo nyara za serikali pamoja na pikipiki zilizokuwa zinatumika kwa wizi.

“Tumefanikiwa kukamata vitu na vielelezo mbalimbali kama ifuatavyo, jumla ya pikipiki 8 ambazo zilikuwa zinatumika kwa wizi au za wizi zilikamatwa, Bangi kilo kumi na kete 278, tulikamata nyara za serikali ambazo ni mikia 21 ya Nyumbu, maganda 5 ya Mayai ya Mbuni, ngozi moja yap aka pori, kipande kimoja cha ngozi ya mbuzi mawe, Miiba 44 ya Nungunungu , vipande vitatu vya mkonga wa tembo, Mikia mitatu ya Ngiri, vipande vitatu vya magamba ya Kobe, kucha tano zap aka pori, kipande kimoja cha jino la Tembo, kipande kimoja cha ngozi ya Fungo pamoja na kipande kimoja cha pembe ya Korongo”.ametaja kamanda Magomi

“Vile vile tuliweza kukamata Meter moja ya Tanesco, Solar panel moja, Control box moja ya mtambo, Tv nne, Subwoofer moja, mafuta ya Petrol lita 225, bidhaa mbalimbali za dukani, seti moja ya mziki wa disko, pombe kali za aina mbalimbali, pombe ya moshi lita kumi, Computer moja, Godoro moja, viti 10 vya plastic, nyaya za miundombinu ya mawasiliano ya TTCL, vyuma vya miundombinu ya barabara, madumu 42 yaliyotaka kutumika katika wizi wa mafuta huko maeneo ya Seke pamoja na Battery mbili kubwa za gari”.amesema kamanda Magomi

“Lakini pia jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga tuliokota pokipiki 9 ambazo kwa namna moja ama nyingine zilisahaulika au kutupwa katika maeneo mbalimbali kutokana na sababu tofauti ikiwa ni pamoja na uhalifu na ulevi”.

“Kesi moja ya kubaka ilihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, kesi moja ya ukatili wa motto ilihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela, kesi moja ya ushirikiana ilihukumiwa kifungo cha nje miezi sita, kesi moja ya uvunjaji ilihukumiwa kifungo cha miezi sita jela pamoja na kesi mbili za kupatikana na Bangi zilihukumiwa kifungo cha miezi sita jela”.amesema Magomi

Katika hatua nyingine Kamanda Magomi amekemea watu wanaojihusisha na lamri chonganishi ambazo zimetajwa kuwa chanzo cha vitendo vya ukatili katika jamii.

TAZAMA VIDEO HAPA CHINI

Post a Comment

Previous Post Next Post