Mwenyekiti wa vijana wakatoliki wafanyakazi VIWAWA
kanda ya ziwa Baraka Masai Shilolelo amewakumbusha viongozi kutoka kwenye
majimbo pamoja na walezi wa VIWAWA kanda hiyo kuimarisha umoja wao katika
kumtumikiwa Mungu kwa kutanguliza maslahi ya kanisa.
Ameyasema hayo kwenye kikao cha mwanzo wa mwaka 2023 cha viongozi mbalimbali wa VIWAWA na walezi wa
majimbo kanda ya ziwa ambacho hufanyika mara mbili kwa Mwaka kwa lengo la kujadili
dira ya Mwaka pamoja na utekelezaji wa maazimio ya VIWAWA Taifa..
Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa vijana ceter mjini Shinyanga
ambapo pamoja na mambo mengine Shilolelo amewasisitiza viongozi hao kuendelea
kushirikiana katika shughuli mbalimbali
ili kuimarisha utume wao kwa ajili ya mafufaa ya kanisa.
“Niwasihi
viongozi wenzagu tusiwasaidie vijana tunaowaongoza kulalamika tuwape majibu
sahihi ya maswali yao viongozi sahihi ni wale wanaotoa majibu ya wale
wanaowaongoza kwahiyo nawaomba sana tusitangulize misimamo yetu tutangulize
maslahi ya wale tunaowaongoza tupendane, tuheshimiane, tusaidiane lakini
tuhurumiane pia maana kila kitu tunachokifanya nikwa ajili ya kristo kusaidiana
kuwe ni sehemu ya maisha yetu lakini ushirikiano utatufikisha kwa kristo kama
matarajio yetu”.amesema Mwenyekiti Shilolelo
Katika kikao hicho viongozi na walezi wa VIWAWA
kutoka majimbo mbalimbali ya kanda pamoja na mambo mengine wametoa ushauri wao
ikiwemo VIWAWA kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya manufaa ya
Kanisa.
Viongozi wa VIWAWA kanda ya Ziwa wamefanya kikao cha Mwanzo wa Mwaka kwa ajili ya
kujadili mambo mbalimbali ikiwemo mkutano utakaofanyika mwezi wa nne pamoja na
kongamano la kanda litakalofanyika mwezi wa sita Mwaka huu 2023.
Kikao hicho kimehudhuriwa na viongozi wa VIWAWA
kutoka majimbo mbalimbali ikiwemo jimbo
katoliki la Shinyanga, jimbo katoliki la Musoma, jimbo katoliki la
Rulenge Ngara, jimbo katoliki la Geita pamoja na viongozi kutoka jimbo kuu
katoliki la Mwanza.
Baadhi ya viongozi hao ni pamoja na Padre Emmanuel
Lyanga mlezi wa VIWAWA kanda ya Ziwa, Padre Peter Mkunya Lyuba mlezi wa VIWAWA
jimbo la Shinyanga, Padre Pamphilius Kitondo John mlezi wa VIWAWA jimbo la
Rulenge Ngara, makamu Mwenyekiti kanda ya Ziwa Gerald Charles Msoke, katibu wa
VIWAWA kanda ya Ziwa John Robert Melli, katibu msaidizi VIWAWA kanda ya Ziwa Suzana
Daud, mhasibu VIWAWA kanda ya Ziwa Steve Simon Mlioo, Mwenyekiti VIWAWA jimbo
katoliki la Geita Musa Masolwa, Mwenyekiti VIWAWA jimbo katoliki la Shinyanga
Leonard Mapolu,
Post a Comment