" BABA MTAKATIFU FARANCISCO, AMTEUA ASKOFU MKUU PROTACE RUGAMBWA, KUWA ASKOFU MKUU MRITHI WA JIMBO KUU LA TABORA.

BABA MTAKATIFU FARANCISCO, AMTEUA ASKOFU MKUU PROTACE RUGAMBWA, KUWA ASKOFU MKUU MRITHI WA JIMBO KUU LA TABORA.


Baba Mtakatifu Farancisco, amemteua Askofu Mkuu PROTACE RUGAMBWA, kuwa Askofu Mkuu mrithi wa Jimbo kuu la Tabora.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Padre Charles Kitima, uteuzi huo umefanyika leo tarehe 13.04.2023.
Mnamo mwaka 2002 hadi 2008, aliombwa kwenda kusaidia kutoa huduma za kichungaji kwenye Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu, utume ambao aliufanya kwa ufanisi mkubwa ambapo tarehe 18 Januari 2008, Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, akamteua kuwa ni Askofu wa Jimbo Katoliki Kigoma, na kuwekwa wakfu tarehe 13 Aprili 2008.
Aidha,mnamo Juni 16 mwaka 2012, Baba Mtakatifu Benedict wa 16 alimteua kuwa Katibu mkuu msaidizi wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu na Rais wa Mashirika ya Kimissionari ya Kipapa mjini VATICAN ambapo amehudumu mpaka alipoteuliwa kuwa Askofu Mkuu mrithi wa Jimbo kuu Tabora.

Post a Comment

Previous Post Next Post