
Na Elisha Petro, Misalaba Media
Klabu bingwa barani Africa (CAF) inarejea hii leo Ijumaa tarehe 16/02/2024 saa nne kamili usiku (10:00 PM) kwa mchezo wa kundi D wenyeji CR Belouizdad kuwakaribisha Al Ahly katika dimba la Stade du 5 Juillet 1962, al- jazair nchini Algeria.
CR Belouizdad wanaingia katika mchezo huo wakiwa nafasi ya tatu baada ya kukusanya alama nne kwenye michezo yao mitatu waliyocheza, wameshinda mchezo mmoja dhidi ya Young Africa (3-0) ,sare mchezo mmoja dhidi ya Al Ahly (0-0) na kupoteza mbele ya Madeama SC kwa goli (2-1 ).
Al Ahly wanaongoza kundi hilo wakiwa na alama tano kwenye michezo mitatu waliyocheza,wameshinda mechi moja dhidi ya Medeama SC (3-0), sare michezo miwili dhidi ya Young Africa (1-1) na CR Belouizdad (0-0).

Post a Comment