Na Mapuli Kitina Misalaba
Baadhi ya wafanya Biashara wakiwemo mama
lishe Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga,
wameitaka serikali kuchukua hatua za haraka kutatua changamoto ya upungufu wa Sukari
ambayo imechangia kuwepo mfumko wa bei.
Wameyasema hayo kwa nyakati tofauti
wakati wakizungumza na Misalaba Media ambapo wameeleza kuwa hivi karibuni bei ya Sukari
imepanda kutoka elfu 2800 hadi elfu nne (4000) kwa kilo moja na kwamba
upatikanaji wake ni mgumu.
Wamesema hatua hiyo imechangia kupungua
kwa wateja na kuathiri mapato katika Biashara zao za kila siku huku wakiiomba
serikali kushughulikia changamoto hiyo haraka ili kuondoa usumbufu
unaojitokeza.
Kaimu afisa Biashara Wilaya ya Kishapu
Albano Mayuma amesema serikali imejipanga kuhakikisha inathibiti mfumko wa bei
ya Sukari na kwamba wafanyabiashara wanaouza kinyume na maelekezo ya serikali
watachukuliwa hatua kali za kisheria
“Hii
changamoto imekuwa ni kubwa kuanzia kwa mfanyabiashara mkubwa hadi mdogo
wanalalamika ukija kwa watumiaji hasa wa majumbani nao wanalalamikia suala la
upatikanaji lakini pia mfumko wa bei, sisi kama serikali tumejiandaa
kuhakikisha kwamba tunadhibiti huu mfumko na kuhakikisha kwamba upatikanaji wa
Sukari unakuwepo walau kwa ile bei ambayo imeelekezwa na bodi ya Sukari lakini
pia tunatoa rai kwa wafanyabiashara ambao wanapandisha bei ya Sukari na wengine
wanaficha Sukari tunawataka wasifanye kitendo hicho maana ni kosa la kisheria
tukiwabaini hatua kali za kisheria zitachukuliwa juu yao ikiwa ni pamoja na
kuwapiga faini”amesema Mayuma
Post a Comment