Na Mapuli Kitina Misalaba
Wakristo na jamii kwa ujumla wametakiwa kumshirikisha
Mwenyezi Mungu katika masuala ya kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Hayo yamebainishwa na
kikundi cha wainjilisti wa makanisa ya Africa Inland Church Tanzania (AICT) Manispaa ya Shinyanga ambao
wanaendelea na maombi maalum ya kuombea mambo mbalimbali ikiwemo ukatili na
kuombea amani Nchini.
Mwenyekiti wa kikundi
hicho Martha Mayunga ambaye ni mama Mchungaji pamoja na Mwinjilisti Hosea
Seronga pamoja na mambo mengine wamesema sambamba na kutoa taarifa za ukatili
kwenye mamlaka husikia ni vema
kumshirikisha pia Mwenyezi Mungu katika maombi ya kila siku.
Katika mahubiri yake ya
leo Mwinjilisti Salome Seronga amewakumbusha wakristo kuendelea kumtumaini
Mungu katika Maisha ya kila siku bila kujali changamoto zinazojitokeza.
Wainjilisti wa makanisa ya AICT Manispaa ya Shinyanga wamekuwa na utaratibu wa kufanya maombo maalum kila mwezi kuombea mambo mbalimbali wakiwemo viongozi wa Dini, Serikali na Taifa kwa ujumla ambapo leo maomba yamefanyika katika Kanisa la AICT Pastoreti ya Ngokolo.
Post a Comment