" MWENYEKITI WA SMAUJATA MKOA WA SHINYANGA AONYA JAMII KUWAADHIBU VIKALI WATOTO

MWENYEKITI WA SMAUJATA MKOA WA SHINYANGA AONYA JAMII KUWAADHIBU VIKALI WATOTO

Mwenyekiti wa kampeni ya shujaa wa maendeleo na ustawi wa jamii Tanzania (SMAUJATA) Mkoa wa Shinyanga Bi. Nabila Kisendi amewataka wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kuacha kuwatendea ukatili watoto ikiwemo kuwaadhibu kupita kiasi.

Ametoa rai hiyo baada ya kutembelea familia ya mtoto anayesadikiwa kufanyiwa ukatili kwa kuadhibiwa vikali na baba yake mdogo ambapo mtoto huyo anasoma katika shule ya msingi Itogwaholo kata ya Isaka Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga.

Imeelezwa kuwa mtoto huyo aliyesadikiwa kufanyiwa ukatili na baba yake mdogo alikuwa anaamshwa saa kumi na moja alfajili kufanya kazi hapo nyumbani na kusababisha kuwa anachelewa shuleni kila siku.

Pia imeelezwa kuwa mwanafunzi huyo alikuwa akisinzia darasani mara kwa mara ambapo walimu wake katika Shule ya msingi Itogwaholo kata ya Isaka walizungumza naye na kubaini changamoto anazopitia na kwamba walimwita huyo mlezi baba yake mdogo nakumonya.

Baada ya kuonywa mlezi huyo bado aliendelea kumfanyia ukatili ikiwemo kumuadhibu vikali ambapo mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Mwalimu Nabila Kisendi alipigiwa simu ambapo alienda kumshuhudia mtoto huyo akiwa ameongozana na viongozi wengine mbalimbali akiwemo afisa maendeleo ya jamii wa kata ya Isaka na kwamba tayari mtuhumiwa huyo amefikishwa kwenye vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua zaidi.

Mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Bi. Nabila Kisendi ametumia nafasi hiyo kuwasisitiza wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kuacha kuwafanyia  ukatili watoto ikiwemo kuwaadhibu kupita kiasi hali hiyo ni ukatili wa kimwili na huathiri kisaikorojia.

SMAUJATA ni kampeni ya kupinga ukatili ambayo inatekeleza majukumu yake chni ya wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi maalum ambapo viongozi wa SMAUJATA Mkoa wa shinyanga wameendelea kuibua na kutoa elimu ya ukatili kwenye jamii na taasisi mbalimbali.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post