" WAJUMBE WA TUGHE SHINYANGA WAKUTANA KUJADILI MIKAKATI YA KUIMARISHA CHAMA

WAJUMBE WA TUGHE SHINYANGA WAKUTANA KUJADILI MIKAKATI YA KUIMARISHA CHAMA

Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Allan Masanja akifungua mkutano mkuu Agosti 20,2024.

Na Mapuli Kitina Misalaba

 Wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) Mkoa wa Shinyanga leo Agosti 20,2024 wamekutana katika ukumbi wa mikutano wa Liga Hotel, Manispaa ya Shinyanga, kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha chama hicho na kuboresha ustawi wa wafanyakazi wa umma katika mkoa huo.

Mkutano huo, ambao hufanyika kila baada ya Miaka miwili na nusu, wajumbe kutoka sehemu mbalimbali za mkoa wa Shinyanga wamehudhuria.

 Katibu wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga Bwana. Ramadhan Pangara, amesoma taarifa ya utendaji wa chama kwa kipindi cha kuanzia Oktoba 2021 hadi Julai 2024, akieleza kuwa chama hicho kwa sasa kinajivunia kuwa na jumla ya wanachama 1,702.

“Mkoa wa Shinyanga kwa sasa tuna wanachama 1,702. Hii ni kutokana na juhudi za kuongeza wanachama wapya na pia kupungua kwa idadi kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo kustaafu hata hivyo, tutaendelea kuongeza idadi ya wanachama na kuboresha huduma kwa wanachama wetu,” amesema Pangara.

Katibu huyo amebainisha mafanikio ya chama katika utetezi wa wafanyakazi, akieleza kuwa TUGHE Mkoa wa Shinyanga imeweza kutoa huduma za utetezi kwa watumishi 25 walioshtakiwa kwa makosa ya nidhamu, huku wanne wakiendelea kupatiwa huduma za kisheria katika mashauri ya jinai.

“Tumefanikiwa kurudisha kazini watumishi watatu, na pia tumehamasisha waajiri kutoa zawadi za wafanyakazi bora kwa wakati tutaendelea kutoa elimu kwa wafanyakazi ili kuepuka matukio yanayopelekea kuchukuliwa hatua za nidhamu na jinai,” amesema Katibu Pangara.

Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Allan Masanja, amesisitiza umuhimu wa wajumbe wa mkutano huo kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kuwahamasisha watumishi wa umma kufuata sheria, kanuni, na taratibu za nchi.

Amewahimiza wajumbe kuwa mstari wa mbele katika kupambana na rushwa mahali pa kazi, akiamini kuwa mkoa wa Shinyanga unaweza kuweka rekodi nzuri katika vita dhidi ya rushwa.

“Msisahau kuzungumzia rushwa mahala pa kazi si kuzuia migogoro tu, rushwa ni mbaya hasa mahali pa kazi nina imani tutavunja rekodi kwa mkoa wa Shinyanga kwa mwaka huu na miaka ijayo, tusiwe na mtumishi ambaye anatuhumiwa kwa rushwa na ukiukwaji wa kanuni na taratibu za watumishi wa umma,” amesema Dkt. Masanja.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati za Wanawake wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga, Experantia Misalaba, ameeleza kuwa kamati hiyo imebuni miradi mbalimbali yenye lengo la kuinua hali ya kiuchumi ya wanachama, ikiwa ni pamoja na vikundi vya vikoba vinavyosaidia wanachama kujikopesha kwa riba nafuu ili kuepuka mikopo yenye riba kubwa.

Katibu wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga Catherine Masalu amehitimisha kwa kuwahimiza watumishi wengine, hususan wale wapya, kujiunga na chama hicho ili kunufaika na huduma na mikakati ya chama.

Mkutano mkuu wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga  umehitimishwa kwa wajumbe kuahidi kuendelea kutekeleza majukumu yao ipasavyo na kuwasisitiza watumishi wote kushirikiana kwa karibu ili kuimarisha utendaji na kuepusha migogoro kazini.

Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Allan Masanja akizungumza kwenye  mkutano mkuu TUGHE Agosti 20,2024.Katibu wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga Bwana. Ramadhan Pangara akisoma taarifa ya kazi ya chama kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Oktoba 2021 hadi Julai 2024 Mkoa wa Shinyanga. 

 Katibu wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga Bwana. Ramadhan Pangara akisoma taarifa ya kazi ya chama kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Oktoba 2021 hadi Julai 2024 Mkoa wa Shinyanga. 

 Katibu wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga Bwana. Ramadhan Pangara akisoma taarifa ya kazi ya chama kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Oktoba 2021 hadi Julai 2024 Mkoa wa Shinyanga. 

Mwenyekiti wa Kamati za Wanawake wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga, Experantia Misalaba akizungumza kwenye mkutano mkuu Agosti 20,2024.

Mwenyekiti wa Kamati za Wanawake wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga, Experantia Misalaba akizungumza kwenye mkutano mkuu Agosti 20,2024.

Katibu wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga Catherine Masalu akizungumza kwenye mkutano mkuu Agosti 20,2024.

Katibu wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga Catherine Masalu akizungumza kwenye mkutano mkuu Agosti 20,2024.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post