" MBUNGE KATAMBI AWASHUKURU WANASHINYANGA KWA USHINDI WA CCM KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024

MBUNGE KATAMBI AWASHUKURU WANASHINYANGA KWA USHINDI WA CCM KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024

Na Mapuli Kitina Misalaba

 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka na ushindi mkubwa kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika hivi karibuni katika jimbo la Shinyanga Mjini, kwa kujinyakulia mitaa 55, vijiji 17, na vitongoji 83 kati ya jumla ya vitongoji 84 vilivyoshindaniwa.

Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa, CCM imepata ushindi wa asilimia 99.3, huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikibeba nafasi moja pekee kwenye kitongoji kimoja, sawa na asilimia 0.7 ya kura zote.

Katika kata mbalimbali za Shinyanga Mjini, matokeo yalionyesha nguvu kubwa ya CCM, ikiwemo:

  • Kata ya Ngokolo (mitaa 7)
  • Ndala (mitaa 5)
  • Kambarage (mitaa 6)
  • Old Shinyanga (vitongoji 13)
  • Ibadakuli (vitongoji 21, huku CCM ikibeba 20 na CHADEMA 1).

Mbunge wa Shinyanga Mjini, Mhe. Paschal Katambi, amewashukuru wakazi wa Shinyanga kwa imani yao kubwa kwa CCM na kuahidi kuendelea kushirikiana nao katika kuwaletea maendeleo endelevu.

"Asanteni wanashinyanga nawaahidi maendeleo zaidi” amesema Katambi.

Kwa ujumla, uchaguzi wa mwaka huu umeonyesha dhamira ya wananchi ya kuendelea kuamini Chama Cha Mapinduzi katika kusimamia maendeleo ya Shinyanga.


Post a Comment

Previous Post Next Post