" MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA WAZAZI TAIFA, HATIBU MGEJA AJITOSA UDIWANI KATA YA NGOKOLO

MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA WAZAZI TAIFA, HATIBU MGEJA AJITOSA UDIWANI KATA YA NGOKOLO


Na Mapuli Kitina Misalaba

Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Wazazi Taifa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hatibu Mgeja, leo Juni 30, 2025, ameonyesha dhamira ya kuwatumikia wananchi kwa karibu zaidi baada ya kuchukua na kurejesha fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kuwania nafasi ya udiwani katika Kata ya Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga.

Hatibu Mgeja amekabidhiwa fomu hiyo katika Ofisi za CCM Kata ya Ngokolo na kaimu katibu wa chama kata hiyo.

Akizungumza mara baada ya kurejesha fomu, Mgeja amesema uamuzi wake wa kuwania nafasi hiyo umetokana na nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi kwa karibu zaidi na kuhakikisha changamoto zinazowakabili zinapatiwa majibu ya haraka kwa ushirikiano kati ya uongozi na jamii.

Zoezi la uchukuaji na urejeshaji fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CCM linaendelea maeneo mbalimbali nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.












Post a Comment

Previous Post Next Post