" MWALIMU KACHE ACHUKUA FOMU YA KUWANIA UDIWANI KATA YA IBADAKULI, AMPONGEZA RAIS SAMIA

MWALIMU KACHE ACHUKUA FOMU YA KUWANIA UDIWANI KATA YA IBADAKULI, AMPONGEZA RAIS SAMIA

Na Mapuli Kitina Misalaba

Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka Mtaa wa Maghorofani, Bugweto, Kata ya Ibadakuli, Mwalimu Naomi Kache, amejiunga rasmi kwenye mchakato wa kuwania nafasi ya udiwani wa Kata ya Ibadakuli, baada ya kuchukua fomu leo Juni 30, 2025, katika ofisi za CCM kata hiyo.

Naomi amesema amechukua uamuzi huo kwa dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi wa Ibadakuli kwa uaminifu, uwazi na uadilifu, endapo chama chake kitampa ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao.

Amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa namna anavyoongoza nchi kwa hekima, busara na kuhimiza usawa wa kijinsia katika uongozi, Naomi amesema ametiwa moyo na hatua za Rais Samia kuwaamini wanawake katika nafasi mbalimbali za maamuzi.

Mchakato wa uchukuaji wa fomu ndani ya CCM unaendelea katika kata na Wilaya mbalimbali mkoani Shinyanga kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.

Naomi Kache, kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), akipokea fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kuwania nafasi ya udiwani Kata ya Ibadakuli, Manispaa ya Shinyanga, katika ofisi za CCM kata hiyo leo Juni 30, 2025.Naomi Kache

Post a Comment

Previous Post Next Post