" VICTOR MKWIZU ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UDIWANI KATA YA NGOKOLO

VICTOR MKWIZU ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UDIWANI KATA YA NGOKOLO

Na Mapuli Kitina Misalaba

Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga, Victor Mkwizu, leo Juni 29, 2025, amejitokeza rasmi kuchukua fomu ya kuwania tena nafasi ya udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mkwizu aliwasili katika ofisi za CCM Kata ya Ngokolo kwa kutumia usafiri wa bodaboda, kitendo kilichoashiria ukaribu wake na wananchi na maisha halisi ya watu wa kawaida anaowawakilisha.

Fomu hiyo amekabidhiwa na Kaimu Katibu wa CCM Kata ya Ngokolo, Jafari Juma, mbele ya wanachama na wafuasi wa chama hicho waliomsindikiza kwa hamasa kubwa.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu, Mkwizu amesema ameamua kutetea nafasi hiyo kwa lengo la kuendeleza jitihada za maendeleo alizozianzisha katika kipindi cha miaka mitano aliyohudumu tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

“Nikipewa ridhaa ya chama kuendelea kupeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu, nitazungumza kwa kina mambo ambayo nimeyafanya kwa ajili ya wananchi wa Ngokolo na mikakati ya kuendeleza pale tulipoishia,” amesema Mkwizu.

Zoezi la uchukuaji fomu kwa nafasi za udiwani linaendelea maeneo mbalimbali nchini huku wagombea mbalimbali wakiendelea kujitokeza kutafuta ridhaa ya chama kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

 

Post a Comment

Previous Post Next Post