" VICTOR MKWIZU AREJESHA FOMU KUWANIA UDIWANI NGOKOLO, ASEMA ANAREJEA KUENDELEZA MAENDELEO

VICTOR MKWIZU AREJESHA FOMU KUWANIA UDIWANI NGOKOLO, ASEMA ANAREJEA KUENDELEZA MAENDELEO

Na Mapuli Kitina Misalaba

Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Ngokolo, Victor Mkwizu, leo Julai 1, 2025, amerejesha rasmi fomu yake ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuwania tena nafasi ya udiwani wa kata hiyo katika uchaguzi mkuu ujao.

Mkwizu ambaye amehitimisha kipindi chake cha uongozi wa miaka mitano, amesema ameamua kurejea tena kwa nia ya kuendeleza misingi ya maendeleo aliyoweka pamoja na wananchi wa Ngokolo katika kipindi kilichopita.

“Nimerudi kwa sababu bado nina ndoto ya kuiona Ngokolo ikisonga mbele zaidi. Tumefanikisha mambo mengi, lakini bado kuna mengi ya kufanya. Naamini kwa ushirikiano na wananchi, tunaweza,” amesema Mkwizu mara baada ya kurejesha fomu.

Ameongeza kuwa anayo dhamira ya dhati ya kuendelea kutumikia wananchi kwa moyo wa uzalendo, huku akiahidi kuzingatia maadili ya uongozi, ushirikiano na uwazi katika utekelezaji wa majukumu.

Zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu linaendelea ndani ya CCM kote nchini, huku wagombea mbalimbali wakiendelea kujitokeza kuomba ridhaa ya chama hicho katika nafasi za udiwani, ubunge na urais kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.Victor Mkwizu, aliyevaa kofia ya chama.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post