" WATOTO WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJILI YA MOTO TABORA

WATOTO WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJILI YA MOTO TABORA


Na Mwandishi wetu, Misalaba Media

Watoto watano wamefarikia dunia wengine 17 wamenusurika kifo baada ya kuwaka kwa bweni la wasichana  kwa kushika  moto katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Igambilo kilichapo kata ya Misha  manispaa Tabora Mkonia hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari mkurungezi wa kituo hicho na mwasisi wake Halima Laswai alisema kwamba kituo tukio lilitokea mida ya saa 5 usiku baada ya kudai kutokea shot ya umeme.  

Alisema kwamba mara baada ya kupata taarifa hiyo alipinga simu kituo cha kizima moto na kutoa ushiriiano kwa ajili ya kuzima moto huo.

Alisema kwamba wakazi wa kijiji hicho cha misha walifanya kazi kubwa kwa ajili ya kuzima moto na kuokoa vitu mbalimbali vilivyokuwepo eneo hilo.

Alisema kwamba Chanzo kilikuwa  umeme unawake na kuzima kisha balubo moja kupasuka na kutoa cheche zilizoangukia kwenye moja ya godoro kwenye kitanda na kuzalisha moto uliosambaa .

Halima alisema kwamba vitu mbalimbali vimeteketea na moto vikiwemo vyakula ambavyo vilikuwa upande wa bweni hilo lillilo shika moto.

Alisema vingine ni vifaa vyote vya shule walivyokuwa wanatumia watoto hao kwa ajili ya maosmo vikimo madfutari na sare ,kwani wengi ya watoto wanasoma shule za msingi.

“Watakwenda kuomba uongozi wa shule ya msingi ili watoto hao waweze kutumia nguo za nyumbani kwa ajili ya kuendelea na masomo yao hasa wale walipo kwenye madarasa ya mitihani ambayo ni Darasa la saba na Nne”alisema Halima

Mkurungezi huyo aliaendelea kubainishwa kwamba kutokana na hali hiyo wawalifanikiwa kuokoa maguni mawili ya unga na Mwili ya maharagwe.

Aidha wanaomba wasamalia wema kujitoa kwa ajili ya kuwasidia watoto wao ili waweza kurudia katika hali zao za kawaida kwa ajili ya kupatia vifaa vya shule na chakula

Afisa ustawi wa kituo hicho. Mwajuma Hassani alisema kwamba mida hile ya usiku akiwa amelala upande mwingine wa bweni kwenye kituo hicho alsiia watoto wanapinga kelele za kuomba masaa na kusema moto moto.

Alisema ndipo walipotoka kwenda kwenye bweni lililoshika na moto na kuvunja mlango wa geti na kufanikiwa kuwatoa watoto ila moshi ulikuwa ni mwingi sana .

Alisema walibofika faya walianza zozezi la kuzima moto ila kipindi hicho wenyeji wa eneo hilo walikuwepo kuwasaidia kuzima moto huo  

Alisema kwamba bweni hilo lilikuwa na watoto waliokuwa wanalala ni 23 kati yao walifariki ni 5 na 17 wamenurika na ajili hiyo ya moto.

kamanda wa jeshi la zimamotona  uokoaji mkoani Tabora Mohamed Jihad aliwataja walifarikia kuwani Pili Nasoro (5) Nusra Adam (11)Amina Ismail(7)Tatu Sharif (4) Norata Bakari (5)

Alibainisha kwamba tuki hilo limeleta simazi kubwa katika mkoa wa Tabora licha ya hali hiyo tahadhari zinatakiwa kuchyukuliwa ili kuoka majanga kama hayo.

Alisema kwamba ushari unaotolewa na jeshi hilo lnafuta kuchukuliwa kwa umakini mkubwa ili kuweza kupunguza ajili zinazoweza kusabishwa namoto.

Hata hivyo waliwataka wananchi na Taasisi mbali  mbali kuchukua hatua za tadhari kwa kuangali vifaa kinga kama vinafanya kazi ipasavyo  na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika majengo na nyumba za kuishi

kituo hicho ni kiliazishwa mwaka 1997 kikiwa na watoto 7 tu na sasa kituo hicho kinawatoto wapatao 50 ila waliotoka ni wengi ambao wapo sehemu mbalimbali kwa ajili ya elimu ya juu na kati 

mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post