" WAKAZI 8000 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI KUTOA ZIWA VICTORIA

WAKAZI 8000 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI KUTOA ZIWA VICTORIA

 

                                                   Na Lucas Raphael,Tabora


Mradi wa upanuzi wa majisafi ya Ziwa Victoria toka Makomero hadi Mgongoro utawanufaisha Zaidi ya wakazi 8000 wa vitongoji viwili na kijiji kimoja Wilayani Igunga mkoani Tabora.  

 

Akizungumza kabla ya kuzinduliwa mradi huo uliogharimu Shilingi 840 milioni ambao uliwekewa jiwe la msingi na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Igunga,Iguwasa,Alex Ntonge  alisema unawanufaisha wakazi ambao walikuwa wakihangaika kutafuta maji.

 Alieleza kuwa wakazi wa maeneo hayo wamekuwa wakipata changamoto kubwa ya maji na kuwafanya watumie muda mqingi kuhangaikia maji.

 Kwa sasa alisema adha waliyokuqa nayo wakazi hao imeisha kwani wanapata huduma ya majisafi na salama kupitia mradi huo.

 Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2025,Ismail Ali Ussi,aliipongeza Iguwasa kwa kuhakikisha wakazi wake wanapata maji na kusema kuwa sekta ya maji inafanya kazi nzuri.

 

Alisema Rais Samia Suluhu Hassan amefanya kazi nzuri ya kuhakikisha fedha nyingi zaidi zinaenda sekta ya maji ambayo nayo haijamuangusha kwa kuwa na miradi yenye ubora.

 Alieleza kuwa watumishi wa sekta hiyo wanafanyankazi nzuri sana na hawana budi kupongezwa kutokana na utendaji aao mzuri wa kazi.

 Mkuu wa Wilaya ya Igunga,Sauda Mtondoo alisema kukamilika kwa mradi huo kunafanya wakazi wanaopata majisafi na salama mjini Igunga kufikia asilimia mia moja.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post