" GEITA HOSPITALI YA RUFAA YAENDELEA KUTOA HUDUMA KWENYE MAONESHO YA MADINI

GEITA HOSPITALI YA RUFAA YAENDELEA KUTOA HUDUMA KWENYE MAONESHO YA MADINI


 

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita imeendelea kutoa huduma za bure za upimaji wa macho, masikio na magonjwa mbalimbali katika maonesho ya teknolojia ya madini yanayofanyika mkoani humo, ambayo yanatarajiwa kufungwa leo.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Mfaume Kibwana, alisema kushiriki kwao maonesho hayo kwa mwaka wa tatu mfululizo ni sehemu ya kuthamini na kutambua mchango wa wananchi, hivyo wameamua kurudisha kwao kwa kuwapatia huduma muhimu za kiafya bila malipo.

“Mwamko wa wananchi ni mkubwa sana, wengi wanakuja kupata huduma. Tunashauri waendelee na utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara,” alisema Kibwana.

Naye Daktari Bingwa wa Macho, Gloria Andrew, alisema changamoto kubwa kwa wakazi wengi wa Geita ni aleji ya macho, hali inayosababishwa zaidi na vumbi katika mazingira ya mkoa huo. Alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kupima macho mapema na kuchukua tahadhari ili kuepuka madhara zaidi.

Hospital hiyo pia imepewa tuzo ya mshindi wa kwanza kwa taasisi za afya ambazo zinatoa huduma .



🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA


Post a Comment

Previous Post Next Post