" MJUMBE WA NEC CCM GASPER KILEO ‘GAKI’ AKAGUA UJENZI WA DARAJA LA KASENGA USHETU

MJUMBE WA NEC CCM GASPER KILEO ‘GAKI’ AKAGUA UJENZI WA DARAJA LA KASENGA USHETU

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Gasper Kileo 'Gaki', ametembelea ujenzi wa Daraja la Kasenga linalounganisha Halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga na Wilaya ya Kaliua mkoa wa Tabora.

Daraja hilo ni miongoni mwa madaraja manne yanayojengwa katika Halmashauri ya Ushetu, likiwa na urefu wa mita 80 na thamani ya shilingi bilioni 5.

Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo, MNEC Gaki amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi na ubora wa kazi inayoendelea.

Ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuona na kutatua kero ya wananchi iliyodumu kwa muda mrefu.

“Mradi huu ni ushahidi wa dhahiri wa jinsi Serikali ya CCM inavyosikiliza na kutatua changamoto za wananchi. Kupitia daraja hili, uchumi wa Ushetu utaimarika kwa kuwa sasa linaunganisha mikoa miwili na kurahisisha shughuli za kijamii na kiuchumi,” alisema Gaki.

MNEC Gaki ametembelea eneo hilo leo akiwa njiani kuelekea kwenye mkutano wa kufunga kampeni za Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ushetu kupitia CCM, Ndg. Emmanuel Cherehani, unaofanyika katika kijiji cha Bugomba B, kata ya Ubagwe.

Post a Comment

Previous Post Next Post