" CHALAMILA AFUTA GHARAMA ZA MIILI YA WANAOFARIKI HOSPITALI WAKATI WA MATIBABU

CHALAMILA AFUTA GHARAMA ZA MIILI YA WANAOFARIKI HOSPITALI WAKATI WA MATIBABU

 Na: Bernardo Costantine, Misalaba Media

Serikali kupitia Mkuu wa  Mko wa Dar es salaam imesisitiza kuwa miili ya wagonjwa wanaofariki dunia wakiwa wanapatiwa matibabu hospitalini, itatolewa bila malipo na kwa haraka ili kuwawezesha ndugu na jamaa kufanya taratibu za mazishi bila kukutana na chagamoto yoyote wakati wa mazishi .

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, wakati  akizungumza na  waandishi  wa habari leo jijini hapa ,akitanabaisha  maboresho ya huduma za jamii  jijini Dar es salaam na Tanzania Kwa ujumla.

Aidha amesema hatua hiyo inalenga kupunguza changamoto zinazowakumba wananchi katika kipindi cha majonzi, hususani wale wanaokosa uwezo wa kugharamia huduma mbalimbali baada ya kufiwa na wapendwa wao.

"Lengo ni kuhakikisha wananchi hawapati usumbufu wa ziada wanapokuwa katika kipindi kigumu cha kuondokewa na ndugu zao. Mwili unapaswa kutolewa mara moja ili taratibu za mazishi ziendelee," 

Amesema

 

Post a Comment

Previous Post Next Post