
Klabu ya Al Ahli Tripoli ya Libya inatarajiwa kutuma ofa mpya ya dola za Marekani milioni 2.5 (sawa na Shilingi bilioni 6.4) kwenda kwa Azam FC, ikiwa ni jitihada za mwisho za kumnasa kiungo nyota Fei Toto.
Hii itakuwa ofa ya tatu kutoka kwa klabu hiyo ya Libya, baada ya ofa mbili za awali kukataliwa na uongozi wa Azam FC.
Taarifa zinaeleza kuwa tayari kuna makubaliano binafsi kati ya Al Ahli Tripoli na Fei Toto, ambapo endapo dili hilo litakamilika, nyota huyo atalipwa dola 60,000 kwa mwezi (sawa na Shilingi milioni 153.6).
Sasa macho na masikio yote yanaelekezwa kwa Azam FC kuona kama safari ya Fei Toto itaendelea kusalia Chamazi au kuelekea Libya.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment