
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linapenda kujulisha kuwa limemkamata na linamshikilia Getruda Japhet Lengesela, Mkazi wa Nsalala – Mbalizi ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo [CHADEMA] Wilaya ya Mbeya Vijijini.
Alikamatwa Januari 22, 2026 saa 3:40 usiku eneo la Nsalala katika Mji Mdogo wa Mbalizi kwa tuhuma mbalimbali za kijinai ikiwepo uchochezi.
Upelelezi unakamilishwa ili hatua zaidi za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake.
Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment