Na Mapuli Kitina Misalaba
Mwakilishi
wa Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Afisa Elimu ya Watu Wazima na
Elimu Nje ya Mfumo Rasmi Mkoa wa Shinyanga, Dedan Rutazika, amewahimiza walimu
wa shule za sekondari kuuelewa kwa kina Mtaala Mpya Ulioboreshwa wa Elimu ya
Sekondari na kuutekeleza kwa ufanisi ili kufanikisha malengo ya elimu na kuinua
ufaulu wa wanafunzi.
Rutazika
ametoa wito huo wakati akifungua mafunzo elekezi kwa walimu yaliyoandaliwa na
Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga leo Januari 22,2026, ambayo yamelenga kuwajengea uelewa na kuongeza
uwezo wa walimu katika utekelezaji wa mtaala mpya.
Katika
hotuba yake, ameipongeza Idara ya Elimu Sekondari ya Manispaa ya Shinyanga kwa
kuendelea kuzingatia mabadiliko ya mitaala ya elimu na kuandaa mafunzo
yanayolenga kuwajengea walimu uelewa wa kina juu ya mabadiliko hayo.
Ameeleza
kuwa mabadiliko ya mitaala yanahitaji walimu kuwa na uelewa wa falsafa ya
mtaala, mbinu za kisasa za ufundishaji na namna bora ya kumjenga mwanafunzi
kimaarifa na kivitendo huku akisisitiza kuwa mafunzo elekezi ni nyenzo muhimu
inayowawezesha walimu kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujiandaa ipasavyo kwa
utekelezaji wa mtaala ulioboreshwa.
Kwa upande
wake, Afisa Elimu Taaluma Sekondari wa Manispaa ya Shinyanga, Mwalimu Richard
Makoye, ameeleza kuwa lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwajengea walimu uelewa wa
namna bora ya kuandaa na kutumia zana za kufundishia na kujifunzia kwa
kuzingatia mtaala mpya ulioboreshwa.
Amesema
kupitia mafunzo hayo, walimu wanajengewa uwezo wa kuandaa mipango ya
ufundishaji, kutumia mbinu shirikishi za ujifunzaji na kutathmini umahiri wa
wanafunzi kwa kuzingatia matakwa ya mtaala.
Mwalimu
Makoye ameongeza kuwa uboreshaji wa ufundishaji wa masomo ya sayansi, sayansi
ya jamii na elimu ya biashara ni hatua muhimu katika kuongeza ufaulu na kuwajengea
wanafunzi uwezo wa kufikiri kwa kina, kutatua changamoto na kujitegemea kielimu
na kijamii.
Nao baadhi
ya walimu walioshiriki mafunzo hayo wameishukuru Idara ya Elimu Sekondari ya
Manispaa ya Shinyanga kwa kuandaa mafunzo hayo, wakisema yamewasaidia kuongeza
maarifa na uelewa wao kuhusu mtaala ulioboreshwa, hususan katika masomo ya
kidato cha kwanza na pili.
Wamesema
uelewa walioupata utachangia kuboresha ufundishaji darasani, kuongeza ufaulu wa
wanafunzi na kuwawezesha wanafunzi kufikia ndoto zao za kielimu.
Mafunzo hayo
yamewakutanisha takribani walimu wawakilishi 170 kati ya walimu 496 kutoka
shule 22 za sekondari zilizopo ndani ya Manispaa ya Shinyanga na kwamba yamewahusisha
walimu wa masomo ya sayansi, sayansi ya jamii pamoja na elimu ya biashara, masomo
ambayo ni miongoni mwa nguzo muhimu katika kujenga uelewa, stadi na umahiri wa
wanafunzi kulingana na mabadiliko ya mtaala mpya.
Kupitia
mafunzo hayo, Manispaa ya Shinyanga inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za
kuinua kiwango cha elimu ya sekondari kwa kuwekeza katika rasilimali watu,
hususan walimu, kama nyenzo muhimu ya kufanikisha mabadiliko ya elimu.
Hatua hiyo
inaendana na kaulimbiu ya Manispaa hiyo isemayo “Shinyanga Municipal, Let Us
Push Together,” inayohamasisha ushirikiano wa wadau wote katika maendeleo ya
elimu na ustawi wa jamii kwa ujumla.
Mwakilishi wa Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga na Afisa
Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi Mkoa wa Shinyanga, Dedan
Rutazika, akizungumza na walimu wa shule za sekondari wakati wa ufunguzi wa
mafunzo elekezi ya utekelezaji wa Mtaala Mpya Ulioboreshwa yaliyoandaliwa na
Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Elimu Taaluma Sekondari wa
Manispaa ya Shinyanga Mwalimu Richrad Makoye, akieleza malengo
ya mafunzo elekezi kwa walimu wa shule za sekondari kuhusu mbinu bora za
kufundishia na kutumia zana za kujifunzia chini ya Mtaala Mpya Ulioboreshwa.
Afisa Elimu Taaluma Sekondari wa
Manispaa ya Shinyanga Mwalimu Richrad Makoye, akieleza malengo
ya mafunzo elekezi kwa walimu wa shule za sekondari kuhusu mbinu bora za
kufundishia na kutumia zana za kujifunzia chini ya Mtaala Mpya Ulioboreshwa.

Walimu wa shule za sekondari wakishiriki kwa bidii
mafunzo elekezi yaliyofanyika Manispaa ya Shinyanga, yakilenga kuongeza uelewa
na uwezo wao katika utekelezaji wa Mtaala Mpya Ulioboreshwa wa Elimu ya
Sekondari.

Walimu wa shule za sekondari wakishiriki kwa bidii
mafunzo elekezi yaliyofanyika Manispaa ya Shinyanga, yakilenga kuongeza uelewa
na uwezo wao katika utekelezaji wa Mtaala Mpya Ulioboreshwa wa Elimu ya
Sekondari.

Walimu wa shule za sekondari wakishiriki kwa bidii
mafunzo elekezi yaliyofanyika Manispaa ya Shinyanga, yakilenga kuongeza uelewa
na uwezo wao katika utekelezaji wa Mtaala Mpya Ulioboreshwa wa Elimu ya
Sekondari.


Walimu wa shule za sekondari wakishiriki kwa bidii
mafunzo elekezi yaliyofanyika Manispaa ya Shinyanga, yakilenga kuongeza uelewa
na uwezo wao katika utekelezaji wa Mtaala Mpya Ulioboreshwa wa Elimu ya
Sekondari.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254






















Post a Comment