Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, Ndugu
Jimotoli Jilala Maduka, tarehe 21 Januari 2026 alimwakilisha Katibu wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi kama Mgeni Rasmi katika Kikao
cha Kawaida cha Baraza la Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Mpanda, kikao cha
kufunga mwaka 2025.
Akizungumza katika kikao hicho, Ndugu Jimotoli Jilala
Maduka aliwasisitiza vijana wa CCM Wilaya ya Mpanda kuendelea kuimarisha umoja
na mshikamano wa pamoja katika utekelezaji wa majukumu ya Jumuiya na Chama Cha
Mapinduzi kwa ujumla, akieleza kuwa nguvu ya chama inajengwa kupitia
mshikamano, nidhamu na ushirikiano wa wanachama wake, hususan vijana.
Ndugu Jimotoli alihimiza vijana wa UVCCM kuwa mstari
wa mbele katika kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi, zikiwemo fursa za
ajira, ujasiriamali, mikopo ya vikundi vya vijana na miradi ya maendeleo
inayotolewa na Serikali, akisema vijana wana nafasi kubwa ya kujenga
mustakabali wao kupitia juhudi, maarifa na ubunifu.
Aidha, Ndugu Jimotoli Jilala Maduka alimpongeza Dkt.
Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, kwa uongozi wake thabiti, wenye maono na unaozingatia maendeleo ya
vijana, amani na ustawi wa Taifa.
Pia amesema Serikali inayoongozwa na Rais Samia
imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa vijana kushiriki kikamilifu katika
shughuli za kiuchumi na kijamii, jambo linalopaswa kuungwa mkono kwa vitendo.
Amewasihi vijana wa CCM Wilaya ya Mpanda kuendelea
kulinda heshima ya chama, kuwa mabalozi wazuri wa sera na mwelekeo wa CCM
katika jamii, pamoja na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na
maendeleo ya wananchi huku akisisitiza umuhimu wa nidhamu, maadili mema na
uzalendo kama msingi wa uongozi bora ndani ya chama.
Baadhi ya viongozi wa UVCCM Wilaya ya Mpanda walimshukuru
Mgeni Rasmi kwa ushauri na hamasa aliyotoa, wakiahidi kuendeleza umoja na
mshikamano, kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo na kuimarisha
mchango wa vijana katika kukijenga na kukitetea Chama Cha Mapinduzi.
Kikao hicho cha kufunga mwaka 2025 kinatumika pia kufanya tathmini ya shughuli za UVCCM kwa mwaka mzima, kuweka mikakati ya mwaka 2026 na kuimarisha ushirikiano kati ya jumuiya za CCM Wilaya ya Mpanda kwa ajili ya maendeleo ya chama na wananchi kwa ujumla.


🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
















Post a Comment