Baraza la Wazazi wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mpanda linafanya kikao chake cha kawaida cha
kufunga mwaka 2025 tarehe 14 Januari 2026, kikao ambacho kinaongozwa na
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Mpanda, Ndugu
Pius Buzumalle.
Katika kikao hicho, Ndugu
Pius Buzumalle amewaomba wajumbe wa baraza kuwa na umoja
na mshikamano wa dhati katika kuendeleza na kuimarisha Jumuiya
ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, huku akiwapongeza wajumbe kwa ushirikiano wao
katika utekelezaji wa majukumu ya chama kwa mwaka mzima wa 2025 ambapo
Mwenyekiti huyo ametumia nafasi hiyo kuwasalimia wajumbe na kuwatakia heri ya
mwaka mpya 2026.
Akizungumzia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, Baraza la Wazazi CCM Wilaya
ya Mpanda linakipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa ushindi mkubwa katika ngazi
zote za uongozi ikiwemo Udiwani, Ubunge na Urais ambapo Jumuiya imeeleza
kuridhishwa na matokeo hayo na kuishukuru CCM kwa kuendelea kushika dola.
Katibu wa Jumuiya ya
Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, Ndugu Jimotoli Jilala
Maduka, ameeleza kuwa Jumuiya inaendelea kuwa imara na iko
mstari wa mbele katika kutekeleza majukumu yake ya chama kwa ufanisi na weledi, akisisitiza umuhimu wa kila mjumbe
kutimiza wajibu wake ndani ya Jumuiya na CCM kwa ujumla.
Ndugu Jimotoli ameendelea
kuwasisitiza wajumbe kuimarisha umoja na mshikamano,
pamoja na kushiriki kikamilifu katika kazi za Jumuiya ya Wazazi na Chama Cha
Mapinduzi ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi kwa wanachama wote waliopo
kwenye nafasi mbalimbali za chama. Katika hatua nyingine, Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Mpanda inatoa shukrani za dhati
kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti
wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuibuka mshindi wa
kiti cha Urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2025, na kutamka wazi kuwa “Hongera sana”.
Kikao hicho pia kimejadili
uimarishaji wa uhai wa Jumuiya ya Wazazi,
ambapo Katibu wa Jumuiya amewahimiza wajumbe kuendelea kulipia ada za
wanachama, kutoa hamasa ya uandikishaji wa wanachama wapya na kuendelea kutoa
elimu katika ngazi za matawi, mashina na kata ili kuongeza idadi ya wanachama.
Katika ajenda ya elimu,
Baraza limeelekeza nguvu katika Shule ya Sekondari na
Ufundi Milala, iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda na
kwamba Jumuiya imeendelea kuisemea na kuipambania shule hiyo kwa lengo la
kuhakikisha eneo la shule linapangwa na kupimwa kwa
wakati ili hatimaye shule ipate Hati
Miliki ya Eneo la Shule.
Hatua hiyo imelenga kuweka mazingira rafiki ya
kutafuta mwekezaji mzuri atakayesaidia
kuendeleza mafunzo, sambamba na kurejesha hadhi ya shule hiyo ambayo awali
ilikuwa ya mfano na bora kwa elimu ya sekondari na ufundi.
Aidha, Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Mpanda imeeleza kuridhishwa na mafanikio ya kisiasa
yaliyopatikana katika Uchaguzi Mkuu wa 2025, ambapo jumla ya madiwani 13 na wabunge wawili (2)
kutoka majimbo ya Mpanda Mjini na Nsimbo wanatokana na Jumuiya ya Wazazi.
Mafanikio hayo yametajwa kuwa matokeo ya umoja, mshikamano na hamasa kubwa iliyotolewa kwa wazazi
kujitokeza kugombea nafasi za udiwani na ubunge.
Mwisho wa kikao, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, Ndugu Pius Buzumalle, amelifunga rasmi baraza la kufunga mwaka 2025 kwa kuwashukuru wajumbe wote kwa kuunga mkono mipango na mikakati ya Jumuiya, hususan katika utekelezaji wa mradi wa shule na masuala mengine yaliyojadiliwa katika kikao hicho.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Mpanda, Ndugu Pius Buzumalle, akizungumza kwenye kikao.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, Ndugu Jimotoli Jilala Maduka, akizungumza.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254















Post a Comment