Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nhelegani Manispaa ya Shinyanga wamepatiwa elimu ya kujikinga dhidi ya ajali za barabarani Kwa kuacha kufanya michezo pindi wanapovuka barabara.
Akitoa elimu hiyo Askari Polisi wa Kikosi Cha usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga Sajenti David Ndimila amewasisitiza kukanyana wao Kwa wao pindi wanapoona Kuna mmoja kati Yao akiwa anafanya michezo wakati wa kuvuka barabara.
Aidha Sajenti Ndimila amewaelimisha sehemu sahihi ya kuvukia ambayo ni kwenye alama ya kivuko Cha watembea Kwa miguu na sio kila mtu kuamua kuvuka sehemu anayojisikia yeye ni sahihi kwake.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254


Post a Comment