" SHY TALENT FILMS YAENDELEA NA MAZOEZI YA UTAYARI WA FILAMU NA TAMTHILIA SHINYANGA

SHY TALENT FILMS YAENDELEA NA MAZOEZI YA UTAYARI WA FILAMU NA TAMTHILIA SHINYANGA


Leo Jumamosi Januari 17, 2026, kikundi cha SHY TALENT FILMS kimeendelea na mazoezi ya utayari wa kutengeneza filamu na tamthilia, hatua inayolenga kuendeleza vipaji vya vijana na kuibua vipaji vipya katika Manispaa ya Shinyanga.

Mazoezi hayo yamefanyika katika ofisi za Misalaba Media, Mjini Shinyanga, na kuhusisha washiriki wengi kutoka kwenye kikundi, ikiwa ni pamoja na waigizaji, walimu wa sanaa na viongozi wa kikundi ambapo kila mshiriki amejikita katika kujifunza mbinu za maigizo, uelewa wa script, na maadili ya kazi ya sanaa.

Akizungumza wakati wa mazoezi, Mkurugenzi wa Misalaba Media, Mapuli Misalaba, amesisitiza umuhimu wa nidhamu, mshikamano na ubora wa kazi katika safari ya kuendeleza vipaji.

Mwenyekiti wa SHY TALENT FILMS, Daniel Elimbopo, amewashukuru washiriki wote kwa moyo wao wa kujitolea na kujitambua, huku akisisitiza kuwa mazoezi haya ni hatua ya kwanza kuelekea kutengeneza filamu na tamthilia zenye ujumbe wa kijamii na elimu.

Pia ameeleza kuwa kikundi hiki ni darasa la maisha kwa vijana, si burudani pekee, bali jukwaa la kujenga fikra, uelewa na weledi wa sanaa.

SHY TALENT FILMS ni kikundi cha sanaa kilichoanzishwa na Misalaba Media, chombo cha habari cha mtandaoni kinachotumia sanaa na ubunifu kama nyenzo ya kuelimisha, kuhamasisha na kuibua vipaji vya vijana.

Kwa taarifa zaidi kuhusu shughuli za kikundi hiki, tembelea ukurasa wao wa Instagram: SHY TALENT FILMS.
“Kuibua vipaji leo, Kujenga wasanii wa kesho.”


 

Post a Comment

Previous Post Next Post