" WANANCHI WAUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI KUBORESHA MAZINGIRA YA UTOAJI WA ELIMU

WANANCHI WAUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI KUBORESHA MAZINGIRA YA UTOAJI WA ELIMU


Na Gift Mongi

Moshi

Baadhi ya shule za msingi kongwe katika kata ya Mwika Kusini katika jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro zimeanza kukarabatiwa ikiwa ni michango kutoka kwa wadau wa maendeleo sambamba na wananchi.

Shule hizo zinazoonekana kujengwa miaka mingi iliyopita hivyo kuwa na changamoto mbali mbali kama kuwepo kwa nyufa,kuchakaa kwa sakafu,mabati kutoboka na hata kutokuwa na pasta katika kuta kwenye baadhi ya majengo.

John Tarimo  ni diwani wa kata hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya zoezi hilo alisema kubwa wananchi hao kwa ridhaa yao wamehamua kukarabati shule hizo badala ya kusubiri serikali iwafanyie kila kitu

"Wananchi wamehamasika na wakahamua sasa ni vyema kukarabati shule ili watoto wawe na mazingira mazuri zaidi ya kujifunzia ila ni mwendelezo wao katika kuunga mkono jitihada mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanywa na serikali"alisema Tarimo


Aidha alisema kuwa suala la maendeleo huletwa na wananchi wenyewe na hivyo kwa kuendelea kukarabati shule hizo kunaonesha ni jinsi gani wananchi hao walivyo na mwitikio mzuri wa watoto wao kupata elimu katika mazingira bora.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mawanda Evarist Shirima alisema kubwa jamii kwa sasa ina mwamko katika elimu na katika kudhihirisha hilo ndio maana jamii haijaachia kila kitu kwa serikali

Alisema shule yake ambayo ina jumla ya wanafunzi 75 imeanza kukarabatiwa na kuwa huo ni mwanzo mzuri katika kurudisha hadhi ya shule hiyo na hivyo wadau hao wa maendeleo hawana budi kuendeleza wema wao huo

"Tunaomba wadau wengine waendelee kujitokeza kwani huu ni mwanzo tu na hakika tutaenda kufika mbali maana imefurahishwa kuona jamii ina mwamko na sio kusubiri serikali hata kwa jambo ambalo lipo chini ya uwezo wetu"alisema

Mwisho

Post a Comment

Previous Post Next Post