Na Mapuli Kitina Misalaba
Serikali imesema imeondoa masharti magumu yaliyokuwa
kikwazo kwa vijana kunufaika na mikopo, ikiwamo dhamana isiyohamishika, ili
kupanua wigo wa upatikanaji wa fedha za uwezeshaji kiasi cha Shilingi bilioni
200 zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Ofisi ya Rais – Maendeleo
ya Vijana.
Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais
– Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka, wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la
Vijana Mkoa wa Shinyanga uliofanyika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga,
ambapo alieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuhakikisha vijana wengi zaidi
wanapata mitaji bila vikwazo visivyo vya lazima.
Amesema fedha hizo zimetengwa mahsusi kwa vijana na
zimesambazwa katika sekta mbalimbali zikiwamo Wizara za Mifugo na Uvuvi,
Kilimo, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo, Viwanda na Biashara pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na
Makundi Maalumu.
Kwa mujibu wa Waziri huyo, dhamira ya Rais ni kuona
vijana wanakuwa wabunifu, wachapakazi na wenye uwezo wa kujitegemea kiuchumi.
Ametolea mfano Mkoa wa Mwanza ambako vijana tayari wamenufaika na Sh milioni
200 kupitia mpango huo.
Aidha, ameeleza kuwa Serikali iko mbioni kuanzisha
dawati maalumu la vijana ndani ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
litakaloshughulikia masuala ya kodi kwa vijana, hatua inayolenga kuweka
mazingira rafiki ya ulipaji kodi na uendeshaji wa biashara zao.
Katika kusisitiza dhamira hiyo, Waziri Nanauka amesema
Serikali pia imeendelea kuwekeza katika kuwajengea vijana ujuzi kupitia Mamlaka
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), ambapo Sh bilioni 3 zimetolewa na
vijana wengi tayari wananufaika na mafunzo ya ufundi stadi.
Amewataka vijana kuwa na ndoto, nidhamu ya muda na
kujituma, akibainisha kuwa vijana ni nguvu kazi muhimu inayochangia takribani
asilimia 55 ya uzalishaji nchini.
Uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga umeelezwa kuwa ni sehemu ya mkakati mpana wa Serikali wa kuimarisha mawasiliano ya moja kwa moja na vijana, kuwafikishia taarifa sahihi za fursa na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21, 2026.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Dkt. Kedmon Mapana akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21, 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21, 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21, 2026.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Wakili Julius Mtatiro akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21, 2026.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
























Post a Comment