Meya wa Manispaa, Mheshimiwa Alex Nyabiti, alisisitiza umuhimu wa mjadala wa kina kuhusu taarifa zilizowasilishwa na kamati, ili kila uamuzi uwe na manufaa kwa wananchi na uchumi wa Manispaa.
kamati zilizowasilisha ripoti ni Kamati ya Mipango Miji na Mazingira Kamati ya Fedha
Kamati ya Elimu, Afya na Huduma za Uchumi
Ripoti hizo ziliwasilisha utekelezaji wa majukumu yao ya kipindi kilichopita, huku madiwani wakijadiliana hatua za kuboresha huduma na kuimarisha maendeleo ya Manispaa.
Aidha, Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini, Mheshimiwa Miraji Mgore Kigera, alishauri Kamati ya Fedha kuongeza juhudi katika kufuatilia wadaiwa wa nyuma, kama ilivyopendekezwa na Serikali ya Mkoa, ili kuongeza mapato na kuboresha huduma kwa wananchi.
Diwani wa Kata ya Rwamlimi, Mheshimiwa Peter Bernard, alisisitiza kuongezwa kwa muda wa leseni za vileo ili kuongeza mapato ya Manispaa. Pia aligusia mpango wa kutoa tuzo kwa kushirikiana na Bongo Buzz, lengo likiwa ni kuhamasisha na kuthamini mchango wa wadau katika maendeleo.
Kikao kilikamilishwa kwa Mwenyekiti wa Baraza kusisitiza utekelezaji wa maagizo yote yaliyotolewa.
Mkurugenzi wa Manispaa amelekezwa kushirikiana na wataalamu wake kuhakikisha ufungaji wa kamera za CCTV kwenye ofisi za Halmashauri kwa ajili ya usalama. Pia, baraza limezingatia usafi wa mazingira na kuagiza ukusanyaji wa taka kufanywa kwa wakati. Hatimaye, ujenzi wa machinjio ya kuku Nyasho umeagizwa kuharakishwa ili kuendeleza huduma na shughuli za kiuchumi kwa wananchi.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254







Post a Comment