" MKALIPA AZIDI KUIMARISHA UHAI WA CCM PANGANI

MKALIPA AZIDI KUIMARISHA UHAI WA CCM PANGANI







Na: Mwandishi Wetu, Pangani 


Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Pangani, Nasri Mkalipa, ameendelea na ziara ya Operesheni Samia ikiwa ni mwendelezo wa Jumuiya anayoingoza kuhakikisha uhai wa Chama unaendelea kuimarika zaidi katika Kata zote 14 za wilaya ya Pangani.


Machi 25, 2026, Mkalipa amefanya ziara katika Kata za Kipumbwi na Mikinguni ambapo amekutana na wanachama wa CCM na wananchi hasa vijana ambao amewahimiza kuendelea kukitumikia Chama kwani Chama kipo pamoja nao bega kwa bega kuhakikisha changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi.


"Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ipo kazini kuhakikisha changamoto za vijana zinapatiwa ufumbuzi, anatoa fedha nyingi kwa ajili ya vijana, ni wajibu wenu kama vijana kujiunga katika vikundi ili muweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa na serikali," amesema Mkalipa.


Aidha, Mkalipa amewahimiza vijana kudumisha amani na mshikamano kwani ndiyo nyenzo ya mafanikio. Kwa upande wa vijana, wameishukuru serikali kwa kuleta miradi mingi ya maendeleo katika Jimbo la Pangani inayogusa sekta za elimu, afya, maji, umeme, miundombinu, uvuvi na kilimo.








 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

 
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post