Shirika
la Kivulini kwa kushirikiana na shirika la World Vision
linaendelea kutekeleza mradi wa Grow ENRICH unaolenga kuboresha afya ya
mama na mtoto pamoja na kuhamasisha ushiriki wa wanaume katika masuala ya afya
ya familia.
Moja
ya shughuli za mradi huo imefanyika katika Kata ya Shagihilu, Wilaya ya
Kishapu, mkoani Shinyanga, ambapo wananchi walikutana katika mdahalo maalum
uliolenga kujadili sababu za ushiriki mdogo wa wanaume katika masuala ya afya
ya mama na mtoto pamoja na kutafuta suluhisho la changamoto hiyo.
Akizungumza
katika mdahalo huo, Meneja wa Mradi kutoka shirika la Kivulini Mageni Malulu
alisema kuwa mradi wa Grow ENRICH unafanya kazi katika nyanja mbalimbali
kuhakikisha vifo vya mama na mtoto vinapungua katika jamii.
Alieleza
kuwa mradi huo unafanya kazi kwa karibu na vituo vya afya na zahanati kwa kutoa
mafunzo kwa watumishi wa afya ili kuboresha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
Aidha, mradi huo pia unafanya kazi na wahudumu wa afya ngazi ya jamii pamoja na
kuboresha baadhi ya miundombinu ya vituo vya afya.
Mageni
Malulu aliongeza kuwa mradi huo pia umeanzisha vikundi mbalimbali ndani ya
jamii ikiwemo vikundi vya “Baba Bora” ambavyo vinahusisha wanaume
wanaotoa elimu na kuwa mfano wa kuigwa katika jamii kwa kuhamasisha ushiriki wa
wanaume katika afya ya familia.
“Tunafahamu
katika jamii nyingi baba ndiye mtoa maamuzi makubwa katika familia, hivyo
tunatumia vikundi vya Baba Bora kuwafikia wanaume wengine na kuwahamasisha
kushiriki kikamilifu katika masuala ya afya ya mama na mtoto,” alisema.
Mbali
na vikundi vya Baba Bora, mradi pia unashirikisha vikundi vya wanawake na
mabinti viongozi pamoja na kundi la Sauti ya Umma na Utekelezaji lenye
wajumbe 10 kutoka kila kijiji ambao hufuatilia masuala mbalimbali katika sekta
za afya, kilimo na maendeleo ya jamii.
Katika
mdahalo huo pia walishiriki makundi ya waendesha pikipiki (bodaboda) ambao
wamepewa vizibao vyenye ujumbe wa elimu ya afya ili kusaidia kusambaza ujumbe
huo kwa wananchi wengi zaidi wanaokutana nao katika shughuli zao za kila siku.
Mdahalo
huo ulisimamiwa na Afisa Maendeleo wa Wilaya ya Kishapu Lailat Naimu
Ramadhani, ambaye aliwaongoza wananchi kutoa maoni yao kuhusu sababu
zinazochangia ushiriki mdogo wa wanaume katika masuala ya afya.
Baadhi
ya sababu zilizotajwa na wananchi ni pamoja na tofauti kubwa ya umri kati ya
baadhi ya wanandoa inayosababisha aibu kwa wanaume kuongozana na wake zao
kliniki, hofu ya wanaume kupima afya zao hospitalini, pamoja na mila na desturi
ambazo wakati mwingine zinachangia wanaume kuona kuwa kuwasindikiza wake zao
hospitali ni jambo lisilofaa.
Wananchi
pia walieleza kuwa baadhi ya wanaume wanaathiriwa na mitazamo ya zamani kuwa
wanawake walijifungulia nyumbani bila kwenda kliniki, hivyo wengine huona si
lazima kushiriki katika huduma za afya.
Aidha,
wengine walieleza kuwa kwa muda mrefu elimu nyingi za afya zililenga zaidi mama
na mtoto huku baba akionekana kusahaulika, hali ambayo ilichangia kupunguza
ushiriki wake katika masuala ya afya ya familia.
Akizungumza
katika mdahalo huo, Afisa Lishe wa Wilaya ya Kishapu Amrani Hemedi Iddi
aliwasisitiza wanaume kushiriki kikamilifu katika kipindi chote cha ujauzito wa
wake zao.
Alisema
mara tu mwanamke anapogundulika kuwa mjamzito ni muhimu baba aanze kutoa
ushirikiano wa karibu ikiwa ni pamoja na kumsindikiza kliniki ili kupata
maelekezo muhimu kutoka kwa wataalamu wa afya.
“Baba
ni mfanya maamuzi katika familia, hivyo anapopata taarifa sahihi moja kwa moja
kutoka kwa wataalamu wa afya inasaidia sana katika kuhakikisha mama na mtoto
wanapata huduma sahihi wakati wa ujauzito na hata baada ya kujifungua,”
alisema.
Katika
mdahalo huo pia walikuwepo viongozi mbalimbali wa serikali na jamii akiwemo
Mtendaji wa Kata ya Shagihilu Simoni Lue, ambaye alisimamia zoezi la
kuweka maazimio ya pamoja ya jamii.
Baadhi ya
makubaliano yaliyofikiwa katika mdahalo huo ni pamoja na:
- Wababa kujitolea kuwasindikiza wake
zao kliniki wakati wa ujauzito na wakati wa huduma za afya.
- Wanaume kuacha hofu ya kupima afya
zao na kujitokeza hospitalini kwa ajili ya uchunguzi wa afya.
- Jamii kuachana na mila na mitazamo
inayozuia wanaume kushiriki katika masuala ya afya ya familia.
- Wababa kutoa msaada wa karibu kwa
wake zao wakati wa ujauzito, kujifungua na baada ya kujifungua.
- Wanajamii kuendelea kupokea na
kusambaza elimu ya afya ili kulinda maisha ya mama na mtoto.
- Vikundi vya Baba Bora kuendelea
kutoa elimu kwa wanaume wengine katika jamii kuhusu umuhimu wa kushiriki
katika afya ya familia.
Diwani wa Kata
ya Shagihilu Deogratius Nicas pia alitoa hamasa kwa wananchi hasa
wanaume kushiriki kikamilifu katika masuala ya afya ya mama na mtoto.
Alisisitiza
kuwa ushiriki wa baba ni muhimu katika kulinda afya ya familia na kujenga jamii
yenye ustawi.
Mdahalo huo
umeacha mwamko mpya kwa wananchi wa Shagihilu ambapo wanaume wameahidi kuongeza
ushiriki wao katika huduma za afya ili kuhakikisha mama na mtoto wanapata
uangalizi bora na kupunguza hatari ya vifo vinavyoweza kuzuilika.
Kupitia mradi
wa Grow ENRICH, shirika la Kivulini pamoja na World Vision wanaendelea
kuimarisha ushirikiano na jamii ili kuhakikisha kila familia inapata elimu na
huduma bora za afya kwa maendeleo endelevu ya jamii.
Meneja mradi kutoka Shirika la Kivulini, Mageni Malulu akizungumza.
Afisa maendeleo Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Lailat Ramadhani akizungumza.
Afisa lishe kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Bwana Amrani Idd akizungumza.

Maafisa usafirishaji kata ya Shagihilu waliopatiwa vizibao vye ujumbe "Baba akishiriki katika afya na lishe ya familia, mama na mtoto hustawi". SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254



































































Post a Comment