" VIJANA WAHIMIZWA KUTUMIA FURSA YA MITANDAO YA KIJAMII KUJIINUA KIUCHUMI

VIJANA WAHIMIZWA KUTUMIA FURSA YA MITANDAO YA KIJAMII KUJIINUA KIUCHUMI

Na Edington Mukiza Ezron, Misalaba Media

Baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Shinyanga wamewahimiza vijana kutumia mitandao ya kijamii kama nyenzo ya kujikwamua kiuchumi na kuchangamkia fursa mbalimbali za maendeleo zinazopatikana kupitia majukwaa hayo.

Wakizungumza na Misalaba Media kwa nyakati tofauti leo Machi 31, 2026, wananchi hao wamesema matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii yanaweza kuwa chachu ya maendeleo kwa vijana endapo yatatumika kwa malengo chanya.

Mmoja wa wananchi hao, Grace Yona, amesema vijana wanapaswa kuitumia mitandao ya kijamii kujiimarisha katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, elimu, sanaa na michezo, badala ya kuitumia kwa mambo yasiyo na tija.

Ameongeza kuwa kupitia mitandao ya kijamii, vijana wanaweza kujenga mahusiano mapana na watu mbalimbali, jambo linaloweza kuwasaidia kupata fursa na kuongeza kipato.

Kwa upande wake, Yusufu Michael amesema baadhi ya vijana wamekuwa wakitumia vibaya mitandao ya kijamii kwa kuiga tamaduni zisizofaa na kujihusisha na vitendo vinavyokiuka maadili ya Kitanzania, hali inayochangia mmomonyoko wa maadili katika jamii.

Aidha, amesisitiza kuwa wazazi pamoja na serikali wanapaswa kutoa elimu ya matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii ili kuwasaidia vijana kuelewa umuhimu wake na kuepuka matumizi yasiyofaa.

Naye Yohana Edward amesema baadhi ya vijana wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya uhalifu kama wizi, utapeli pamoja na kusambaza maudhui yasiyofaa mtandaoni, jambo ambalo linaweza kuathiri mustakabali wao na kuwafanya wakumbwe na hatua za kisheria.

Kwa upande mwingine, baadhi ya vijana wameiomba serikali kuboresha upatikanaji wa huduma za intaneti kwa gharama nafuu, wakisema gharama za vifurushi vya data ni kubwa na zinawazuia kutumia ipasavyo fursa zilizopo mtandaoni.

Hata hivyo, vijana wametakiwa kutumia mitandao ya kijamii kwa uangalifu na malengo yenye tija, ili kuepuka kuharibu maadili, kuchafua sifa zao pamoja na kujiepusha na athari za kisheria zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi mabaya ya teknolojia hiyo.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

 
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post