Wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East
African Spirits (Super Women GAKI Group) wameadhimisha Siku ya Wanawake Duniani
kwa kufanya hafla maalum ya kusherehekea mchango wa wanawake katika jamii na
mahali pa kazi, huku wakisisitizwa kujiamini, kujitegemea kiuchumi na kudumisha
umoja.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo ni Mkurugenzi Msaidizi
wa kampuni hizo, Gladnes Gasper Kileo, ambaye amesema kuwa maadhimisho hayo ni
ya kwanza kufanyika katika kampuni ya GAKI Investment na yataendelea kuwa
utamaduni wa kila mwaka.
“Leo tunaadhimisha Siku ya Wanawake
Duniani, na hili ni tukio la kwanza kufanyika katika kampuni ya GAKI
Investment. Tukio hili litakuwa endelevu na ninaahidi kuwa mwakani
nitalisimamia mwenyewe,” amesema Kileo.
Amesema kuwa wanawake wakipewa nafasi wanaweza kufanya
kazi kwa ufanisi mkubwa katika sekta mbalimbali, akitolea mfano uwepo wa
wanawake katika uongozi wa juu serikalini, biashara na taaluma nyingine ambazo
hapo awali zilikuwa zikitawaliwa zaidi na wanaume.
“Kwenye siasa tuna Rais mwanamke, kwenye
biashara wanawake tupo, hata kazi ambazo zamani zilionekana ni za wanaume kama
uendeshaji wa mitambo au ufundi umeme, sasa wanawake wapo wengi. Hata ndani ya
familia mwanamke anaweza kufanya kazi huku akisimamia familia, jambo ambalo si
rahisi lakini linawezekana,” amesema.
Gladnes amewataka wanawake kuanza kwa kujiamini ili
waweze kufikia malengo yao katika maisha.
“Kumtambua mwanamke anaweza kunaanza na
kujiamini. Kila kitu kinaanza kwenye fikra zako. Ukiamini unaweza, utaweza
kweli; lakini ukiamini huwezi, kamwe hautaweza. Jiwekee malengo na amini
unaweza kuyafikia,” amesisitiza Gladnes.
Aidha amewataka wanawake kujitegemea kiuchumi ili wawe
na sauti ndani ya familia na jamii.
“Mwanamke ukiwa na kipato chako unapata
uhuru wa kufanya maamuzi. Mwanamke asiye na kipato mara nyingi hukosa sauti
katika familia na hata kwenye jamii. Ni muhimu kila mwanamke ajitafutie kipato
chake,” amesema.
Pia amewahimiza wanawake kudumisha umoja na
mshikamano, akisema kuwa utengano unaweza kudhoofisha mafanikio yao.
“Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu.
Shikamaneni, shirikianeni na pendaneni. Hata mkipishana mawazo kumbukeni kuwa
lengo lenu ni moja na mtaweza kusonga mbele,” amesema Gladnes.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Super Women GAKI Group,
Immaculate Temu, amemshukuru mgeni rasmi kwa ushauri na hamasa aliyotoa, huku
akiahidi kuwa wanawake wa kampuni hiyo watazifanyia kazi nasaha hizo.
Temu amesema maadhimisho ya mwaka ujao yatafanyika kwa
kiwango kikubwa zaidi na kwa ubunifu tofauti ili kuendelea kuwainua wanawake
ndani ya kampuni.
Katika hafla hiyo pia kulikuwa na mada mbalimbali za
kuwahamasisha wanawake. Mtoa mada Savela Andrew amewahimiza wanawake kufanya
kazi kwa bidii na kujituma ili waweze kufikia mafanikio binafsi na kusaidia
familia zao.
“Wanawake tunatakiwa kujituma katika kazi,
kwani kazi ni msingi wa maisha. Mwanamke anapofanya kazi kwa moyo wote anaweza
kuhudumia familia yake na kujijengea heshima katika jamii,”
amesema.
Ameongeza kuwa wanawake wanapaswa kuwa na lugha nzuri
kazini, kupendana wao kwa wao na kujithamini.
“Mwanamke lazima ampende mwanamke
mwenzake. Pia tuwe wasafi na tujitunze. Usipojipenda na kujithamini, nani
atakupenda?”.
Naye mfanyakazi wa GAKI Investment, Lucy Kimati, amezungumzia
kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inayosema “Haki na Usawa kwa Wanawake na
Wasichana: Msingi Jumuishi Kufikia Dira 2050.”
Amesema mwanamke ana mchango mkubwa katika maendeleo
ya jamii kwa kuwa anasimamia familia na wakati huo huo kushiriki katika
shughuli za uzalishaji.
Kimati pia amempongeza mkurugenzi wa kampuni hizo kwa
kuzingatia usawa wa kijinsia kwa kutoa nafasi nyingi za ajira kwa wanawake.
“Kipekee kabisa sisi wanawake wafanyakazi
wa GAKI Investment tunamshukuru sana mkurugenzi wetu kwa namna alivyotoa nafasi
kwa wanawake. Katika kampuni hizi wanawake ni wengi, jambo linaloonesha kuwa
suala la usawa wa kijinsia limezingatiwa,” amesema Kimati.
Maadhimisho hayo yamelenga kuhamasisha wanawake
kujiamini, kushirikiana na kutumia fursa zilizopo ili kufikia maendeleo yao
binafsi na ya jamii kwa ujumla.
Kampuni ya GAKI Investment Limited ni miongoni
mwa wawekezaji wakubwa wa viwanda mkoani Shinyanga, ikijishughulisha na
shughuli mbalimbali za uzalishaji na biashara zinazochangia kukuza uchumi wa
wakulima na kutoa ajira kwa wananchi.
Moja ya shughuli kuu za kampuni hiyo ni uchambuzi wa
pamba (cotton ginning) ambapo hununua pamba kutoka kwa wakulima katika mikoa ya
Shinyanga, Simiyu na maeneo ya jirani kisha kuichambua katika kiwanda chake
kilichopo mkoani Shinyanga.
Mbali na uchambuzi wa pamba, kampuni hiyo pia
inajishughulisha na uzalishaji wa mafuta yatokanayo na mbegu za pamba, pamoja
na shughuli nyingine za viwandani zikiwemo uzalishaji wa mifuko ya plastiki ya
kufungashia bidhaa na uwekezaji katika sekta ya biashara.
Kupitia uwekezaji huo, kampuni ya GAKI Investment
imekuwa ikitoa ajira kwa vijana na wanawake wengi pamoja na kusaidia wakulima
kupata soko la uhakika la zao la pamba.
Wakati huo huo, kampuni ya East African Spirits (T)
Limited, ambayo pia inahusishwa na uwekezaji wa kundi hilo la kampuni,
inajishughulisha na uzalishaji wa vinywaji vikali (spirits) vinavyotengenezwa
viwandani na kusambazwa katika maeneo mbalimbali nchini na nje ya nchi.
Kampuni hiyo huzalisha aina mbalimbali za bidhaa za
vinywaji vikali zinazouzwa katika soko la ndani na nje, ambapo imekuwa miongoni
mwa kampuni zinazochangia ukuaji wa sekta ya viwanda pamoja na mapato ya
serikali kupitia kodi.
Baadhi ya bidhaa zinazozalishwa ni pamoja na: Goldberg,
Hanson’s Lite, Diamond Rock, Hanson’s Choice na Basembi.
Uwepo wa kampuni hizo mkoani Shinyanga umeendelea
kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi kwa kutoa ajira, kusaidia
wakulima wa pamba kupata masoko na kuongeza thamani ya mazao kupitia shughuli
za viwanda.
Mkurugenzi Msaidizi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits, Gladnes Gasper Kileo, akizungumza na wanawake wafanyakazi wa kampuni hizo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Mkurugenzi Msaidizi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits, Gladnes Gasper Kileo, akizungumza kwenye hafla hiyo.TAZAMA PICHA MBALIMBALI
Mwenyekiti wa Super Women GAKI Group, Immaculate Temu, akizungumza wakati wa hafla ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani iliyoandaliwa na wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakiwa katika hafla ya kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakiwa katika hafla ya kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakiwa katika hafla ya kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakiwa katika hafla ya kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani.
Wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakisherehekea kwa pamoja maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakisherehekea kwa pamoja maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakisherehekea kwa pamoja maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakisherehekea kwa pamoja maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
TAZAMA PIA PICHA ZA ASUBUHI KABLA YA HAFLA YA USIKU.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakiwa katika picha ya pamoja asubuhi katika ofisi za kampuni hizo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakiwa katika picha ya pamoja asubuhi katika ofisi za kampuni hizo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakiwa katika picha ya pamoja asubuhi katika ofisi za kampuni hizo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakiwa katika picha ya pamoja asubuhi katika ofisi za kampuni hizo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni za GAKI Investment na East African Spirits wakiwa katika picha ya pamoja asubuhi katika ofisi za kampuni hizo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254



















































































Post a Comment