" ASKOFU CHINYONGOLO ASISITIZA MALEZI YA KIROHO KAMA MSINGI WA AMANI KWA VIJANA

ASKOFU CHINYONGOLO ASISITIZA MALEZI YA KIROHO KAMA MSINGI WA AMANI KWA VIJANA

 

Askofu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Steven Chinyongolo, amesisitiza umuhimu wa malezi ya kiroho kwa watoto na vijana akieleza kuwa ni msingi muhimu katika kujenga jamii yenye amani, maadili na mshikamano.

Akizungumza katika uzinduzi wa mtaala wa Mama wa Upendo pamoja na program ya Alpha uliofanyika katika Klasta ya Shinyanga, Askofu Chinyongolo amewataka vijana kutumia fursa hiyo kujijenga kiroho na kuwa na hofu ya Mungu ili waweze kuepuka mienendo isiyofaa inayoweza kuhatarisha amani ya jamii.

Kwa upande wake, Mwezeshaji wa Klasta ya Shinyanga na Kahama, Bwana Remi Dumbi, amesema kuwa mtaala huo unalenga kuwawezesha wamama wa upendo kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi katika kuwalea na kuwaombea watoto pamoja na vijana, akibainisha kuwa maombi ni nguzo muhimu katika kujenga kizazi chenye maadili na kinacholinda amani.

Naye Mchungaji Odras amewahimiza washiriki kumtumaini Mungu na kuomba uongozi wake katika utekelezaji wa mtaala huo, akisisitiza kuwa malezi ya kiroho yana mchango mkubwa katika kuimarisha utulivu na amani katika jamii.

Wakati huo huo, wamama wa upendo wa huduma ya Esta Encounter katika Klasta ya Shinyanga wameeleza kuwa wameendelea kushirikiana kwa karibu katika kuwalea na kuwaombea watoto na vijana, wakiamini kuwa kupitia umoja na mshikamano, wataweza kujenga kizazi chenye maadili kitakachodumisha amani ya taifa.

Huduma hiyo, iliyoanzishwa mwaka 2008, inalenga kuwawezesha wanawake kushiriki kikamilifu katika malezi ya watoto na vijana kupitia maombi, ushauri na malezi ya kijamii, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kujenga jamii yenye maadili na amani endelevu.








SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

 
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254


Post a Comment

Previous Post Next Post