Na Mapuli Kitina Misalaba
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi
wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) Mkoa wa Shinyanga, Nabila Kisendi, ametoa wito kwa
wananchi kuendelea kulinda amani na kudumisha mshikamano katika jamii ili
kuhakikisha maendeleo yanaendelea kupatikana.
Akizungumza na Misalaba Media, Kisendi amesema kuwa
amani ni msingi muhimu wa ustawi wa jamii na kwamba bila utulivu, juhudi za
maendeleo haziwezi kufanikiwa.
Amesisitiza umuhimu wa wananchi kushirikiana na
viongozi pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha mazingira
yanaendelea kuwa salama, huku akiwataka kujiepusha na vitendo vinavyoweza
kuhatarisha amani.
Kisendi pia amewahimiza vijana kuwa mstari wa mbele
katika kulinda amani, akibainisha kuwa wao ndiyo nguvu kazi ya taifa na
wanapaswa kutumia nguvu zao katika shughuli za maendeleo badala ya kujiingiza
katika migogoro isiyo na tija.
Aidha, amesema SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga itaendelea
kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa amani, maadili na mshikamano, ikiwa ni
sehemu ya juhudi za kujenga taifa lenye utulivu na maendeleo endelevu.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment