Mwenyekiti wa Jumuiya ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi
wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) Nabila Kisendi, kwa kushirikiana na viongozi wa
Halmashauri ya Msalala wasamaria wema, wamefanikisha zoezi la kumuokoa mtoto
mwenye umri wa miaka miwili aliyekuwa akiishi katika mazingira hatarishi akiwa
na mama yake mwenye changamoto ya afya ya akili katika Kijiji cha Isaka
Station, Kata ya Isaka, Halmashauri ya Msalala, Wilaya ya Kahama.
Tukio hilo lilianza Aprili 11, 2026 ambapo viongozi wa
SMAUJATA wakiongozwa na Mwenyekiti wa Mkoa Bi. Nabila Kisendi, Mwenyekiti wa
Kata Bi. Sophia Emanuel, Pamoja na Katibu wa Halmashauri ya Msalala, Bi. Nives
Nyoni waliinua juhudi za kuokoa familia hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mtoto huyo alikuwa akiishi
katika mazingira yasiyo salama, akilala maeneo mbalimbali pamoja na mama yake,
jambo lililoibua wasiwasi kwa wananchi na viongozi wa eneo hilo.
Baada ya jitihada za siku kadhaa, Aprili 14 majira ya
saa mbili usiku, viongozi hao walifanikiwa kumchukua mtoto huyo kutoka kwa mama
yake na kumpeleka kwa Mwenyekiti wa Kitongoji wa eneo hilo, Mahamud Hamad
maarufu Tolonto, kwa ajili ya usalama wa muda.
Katika kipindi chote cha zoezi hilo, viongozi wa
SMAUJATA walikuwa wakishirikiana kwa karibu na Jeshi la Polisi pamoja na
maafisa ustawi wa jamii wa Halmashauri ya Msalala, akiwemo Richard Jackson
Ignace Lifulila na Madam Magori.
Baadaye, mtoto huyo alifikishwa katika kituo cha
kulelea watoto yatima kilichopo Kagongwa, Wilaya ya Kahama, kwa ajili ya malezi
na uangalizi zaidi.
Aidha, ofisi ya ustawi wa jamii ya Msalala ilisaidia
gharama za usafiri ili kufanikisha zoezi hilo, huku mawasiliano zaidi
yakifanyika na maafisa ustawi hadi kufanikiwa kuwapata ndugu wa mama huyo,
ambao walifika na kumchukua kwa ajili ya uangalizi wa kifamilia.
Viongozi wa SMAUJATA wamewashukuru wote walioshiriki
katika zoezi hilo, wakiwemo viongozi wa eneo, maafisa ustawi wa jamii,
watendaji wa Isaka Station pamoja na wananchi waliochangia fedha na ushirikiano
hadi kufanikisha lengo la kumuokoa mtoto huyo.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment