
Dkt. Meshack Kulwa, Mkurugenzi wa Shirika la Lifeline Cocenselly Centre and Gender Empowerment, akielezea utekelezaji wa mradi wa Safari ya Mpaji Uzima na umuhimu wake kwa jamii.Na Mapuli Kitina Misalaba
Mafunzo ya siku nne ya program ya Safari ya Mpaji-Uzima yamefanyika
katika ukumbi uliopo Kata ya Ndala, Manispaa ya Shinyanga, yakilenga kuwajengea
uwezo viongozi wa dini na wadau mbalimbali kuhusu thamani ya maisha ya
mwanadamu na masuala ya kiroho yanayohusiana na uhai.
Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Mkurugenzi
wa Shirika la Lifeline Cocenselly Centre and Gender Empowerment, Dkt. Meshack
Kulwa, amesema kuwa program ya Safari ya Mpaji-Uzima ni sehemu ya miradi
ya taasisi ya Life International yenye makao yake nchini Marekani, ambayo
ilianzishwa kwa lengo la kupinga utoaji mimba na kulinda uhai wa binadamu.
Amesema Lifeline imefanikiwa kuanzisha ushirikiano na
taasisi hiyo baada ya mawasiliano ya takribani miaka mitatu, hatua iliyowezesha
kuanza rasmi utekelezaji wa program hiyo nchini Tanzania.
“Tumekuja na safari ya mpaji uzima kwa
ajili ya kutengeneza uelewa kwa jamii, na baadaye tutaweka mazingira ya
kuwafikia Watanzania wengi zaidi. Huu ni mwanzo tu, lakini tuna mipango mingine”amesema
Dkt. Kulwa.
Ameongeza kuwa semina hiyo imewakutanisha washiriki
kutoka maeneo mbalimbali nchini, wakiwemo viongozi wa dini za Kikristo na
Kiislamu, akiwataja wachungaji, maaskofu na masheikh kutoka mikoa ya Geita,
Tabora, Dodoma, Shinyanga na Dar es Salaam. Pia mafunzo hayo yamewezeshwa na
wakufunzi kutoka Nairobi nchini Kenya.
Dkt. Kulwa amewasisitiza washiriki kutumia elimu
waliyoipata kwa vitendo katika jamii zao, akiwahimiza kuanzia kwenye nyumba za
ibada na taasisi wanazozisimamia ili kufikisha ujumbe mpana zaidi kwa jamii.
Kwa upande wake, akizungumza kwa niaba ya wawezeshaji
kutoka Nairobi, Mtume Patrick Ngundo amesema mafunzo hayo ni ya muhimu kwa
washiriki kwani wao ndio waliobeba dhamana ya kuifikisha elimu hiyo kwa
wengine.
“Hili tulilopokea ni muhimu sana. Sisi tumewapa elimu
na tunatarajia mkaifikishe kwa wengine kule ambako hatuwezi kuwafikia. Huu ni
mwanzo wa safari, na kwa msaada wa Mungu tutaendelea kushirikiana nanyi,”
amesema Ngundo, akiongeza kuwa wataendelea kuwaombea washiriki na kudumisha
ushirikiano huo.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwemo Pendo
Mashishanga kutoka Kanisa la AICT Kambarage na Kanon Mazugun kutoka asasi ya
kijamii ya PATWA, wameeleza kufurahishwa na mafunzo hayo na kuahidi kuyafanyia
kazi.
“Tunaishukuru sana timu ya wawezeshaji kutoka Kenya
kwa kutupa mafunzo haya. Tunaahidi kwenda kuyafikisha kwa wengine na kufanya
kazi kubwa ya kutoa elimu kwa jamii,” wamesema washiriki hao.
Kwa mujibu wa mtaala wa kimataifa wa Safari ya
Mpaji-Uzima (Toleo 5.1) uliotolewa na Life International, mafunzo hayo
yanajikita katika mada mbalimbali zikiwemo utafiti wa maisha ya mwanadamu,
mtazamo wa kibiblia kuhusu uhai, vita vya kiroho, maombi ya maombezi, familia,
ujinsia wa kibiblia, uzazi, pamoja na athari na hatua zinazohusiana na utoaji
mimba.
Mtaala huo unalenga kuwaandaa viongozi wa Kikristo
kimataifa ili waweze kusimamia na kuhamasisha utunzaji wa uhai wa binadamu kwa
misingi ya kiimani na kijamii.


Mtume Patrick Ngundo, mkufunzi kutoka Nairobi, Kenya, akizungumza na washiriki kuhusu wajibu wa kusambaza elimu waliyoipata kwa jamii.
Mchungaji Margaret Makilya, mkufunzi kutoka Nairobi, Kenya, akitoa shukurani kwa washiriki wakati wa mafunzo hayo.
Mchungaji Esther Patrice, mkufunzi kutoka Nairobi, Kenya, akizungumza na washiriki kuhusu masuala ya kiroho na uhai wa mwanadamu.Collins Kimaro, mkufunzi kutoka Nairobi, Kenya, akizungumza mambo mbalimbali kwa washiriki katika mafunzo ya Safari ya Mpaji Uzima.

Washiriki wa mafunzo ya Safari ya Mpaji Uzima wakikabidhiwa vyeti baada ya kuhitimisha mafunzo ya siku nne yaliyofanyika Kata ya Ndala, Manispaa ya Shinyanga.
Washiriki wa mafunzo ya Safari ya Mpaji Uzima wakikabidhiwa vyeti baada ya kuhitimisha mafunzo ya siku nne yaliyofanyika Kata ya Ndala, Manispaa ya Shinyanga.
Zoezi la utoaji vyeti likiendelea kwa washiriki waliokamilisha mafunzo ya siku nne ya Safari ya Mpaji Uzima.
Zoezi la utoaji vyeti likiendelea kwa washiriki waliokamilisha mafunzo ya siku nne ya Safari ya Mpaji Uzima.
Wawezeshaji wakikabidhi vyeti kwa washiriki waliomaliza mafunzo ya Safari ya Mpaji Uzima yaliyolenga kujenga uelewa kuhusu thamani ya maisha ya binadamu.
Wawezeshaji wakikabidhi vyeti kwa washiriki waliomaliza mafunzo ya Safari ya Mpaji Uzima yaliyolenga kujenga uelewa kuhusu thamani ya maisha ya binadamu.
Washiriki wakipokea vyeti vyao kama ishara ya kukamilisha mafunzo ya siku nne yaliyowakutanisha viongozi wa dini na wadau mbalimbali.
Washiriki wakipokea vyeti vyao kama ishara ya kukamilisha mafunzo ya siku nne yaliyowakutanisha viongozi wa dini na wadau mbalimbali.
Picha ya pamoja ya washiriki na wawezeshaji baada ya kukabidhiwa vyeti kufuatia hitimisho la mafunzo ya Safari ya Mpaji Uzima.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
















































Post a Comment