Mchungaji wa Kanisa la AICT Kambarage, Jonas Mwita, amewahimiza Wakristo kuwa mfano bora katika jamii kwa kusimamia na kulinda amani katika maeneo yao.
Mchungaji Mwita amesema kuwa kila Mkristo ana wajibu
wa kuhakikisha anachangia kudumisha utulivu na mshikamano, akibainisha kuwa
amani ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii.
Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa Wakristo kuchagua
marafiki na watu wanaowazunguka, ili kuepuka ushawishi wa ushauri mbaya
unaoweza kuwapeleka katika matendo yanayohatarisha amani na mustakabali wao.
Aidha, amewahimiza waumini kuendelea kushikamana,
kuheshimiana na kuzingatia maadili mema katika maisha yao ya kila siku,
akieleza kuwa jamii yenye hofu ya Mungu huwa na msingi imara wa amani na
upendo.
Mchungaji Mwita ametoa rai kwa Wakristo na jamii kwa ujumla kuendelea kuwa walinzi wa amani kwa vitendo, ili kuhakikisha utulivu unaendelea kudumu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment