Na Edington Mukiza Ezron, Misalaba Media
Baadhi ya wajasiriamali wa Soko la Mnara wa Voda
wamelalamikia hali ya usafi katika soko hilo, wakiiomba serikali kuajiri
wafanyakazi maalum wa kufanya usafi ili kuboresha mazingira na kupunguza
usumbufu unaowakabili.
Akizungumza na Misalaba Media katika soko hilo, Irene
Pascal amesema licha ya wajasiriamali kuchangia fedha za ukusanyaji taka, bado
hali ya usafi hairidhishi, hivyo kuna haja ya kuwepo kwa mfumo rasmi wa
usimamizi wa usafi kama ilivyo katika masoko mengine.
Aidha, ameeleza kuwa soko hilo linakabiliwa na
upungufu wa vyoo, hali inayoweza kuchochea magonjwa ya mlipuko ikiwemo
kipindupindu, na kuomba mamlaka husika kuchukua hatua za haraka kujenga
miundombinu hiyo muhimu.
Wajasiriamali hao pia wamebainisha kuwa baadhi ya
wafanyabiashara hawazingatii usafi wa mazingira yao, jambo linalochangia
kuzorota kwa hali ya soko. Wamewataka wenzao kushirikiana katika kudumisha
usafi ili kulinda afya zao na kuvutia wateja.
Kwa upande wake, Katibu wa Soko hilo, Samson Marwa,
amekiri kuwepo kwa changamoto hizo na kuziomba mamlaka za afya kutembelea soko
hilo mara kwa mara kwa ajili ya kutoa elimu na kufanya tathmini ya hali ya
usafi.
Hata hivyo, wamezitaka mamlaka husika kuchukua hatua
kali za kisheria dhidi ya wale wanaokiuka taratibu za usafi ili kukomesha
tatizo hilo na kuboresha mazingira ya biashara.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment