Na Mapuli Kitina Misalaba
Baadhi ya Mama Lishe wanaofanya biashara katika kata
ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga wamefunguka kuhusu faida
wanazoendelea kuzipata kupitia mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 huku
wakiitakia timu ya HOME BOYS kutwaa ubingwa wa mashindano hayo mwaka huu.
Wakizungumza na Misalaba Media kwa nyakati tofauti,
Mama Lishe hao wamesema mashindano hayo yamechangia kuongezeka kwa wateja
kutokana na idadi kubwa ya mashabiki, wachezaji na wageni wanaofika kufuatilia
michezo hiyo kila siku.
Wamesema tofauti na siku za kawaida, siku za mechi
huwaletea fursa kubwa ya kuuza vyakula na vinywaji jambo ambalo limewaongezea
kipato na kuwasaidia kuendesha maisha yao ya kila siku.
Aidha wamempongeza mwandaaji wa mashindano hayo, Bwana
Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa kuendelea kuandaa mashindano
yanayokuza vipaji vya vijana huku yakichochea shughuli za kiuchumi kwa wananchi
wa eneo hilo.
Mama Lishe hao pia wameeleza kuvutiwa na kiwango
kinachooneshwa na timu ya HOME BOYS katika mashindano hayo na kuitakia
mafanikio zaidi huku wakiamini inaweza kufika hatua ya mwisho na kutwaa ubingwa
wa NIACHEKONA CUP 2026.
Wameongeza kuwa mashindano hayo yanapaswa kuendelea
kuungwa mkono na wadau mbalimbali kwa kuwa yana manufaa makubwa kwa vijana,
wafanyabiashara na jamii kwa ujumla.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yanaendelea katika
uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa yakihusisha timu mbalimbali kutoka ndani na
nje ya Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kuibua vipaji vya vijana na kukuza
michezo kupitia ufadhili wa Lushu Foundation.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment