Na Mapuli Kitina Misalaba
Jeshi la Polisi kata ya Solwa limepongeza jitihada
zinazofanywa na mdau wa michezo katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Paul
Daud Augustino kwa kuanzisha mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 ambayo
yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuibua vipaji vya vijana pamoja na kuimarisha
amani katika jamii.
Akizungumza katika mashindano hayo yanayoendelea
kwenye uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Polisi Kata wa kata ya Solwa Paul
Mashimba amesema michezo hiyo imekuwa na mchango mkubwa katika kuwaweka vijana
karibu na shughuli za maendeleo badala ya kujihusisha na vitendo visivyofaa
katika jamii.
“Kwanza kabisa namshukuru mdau wa michezo
katika Wilaya hii ambaye ni MC NIACHEKONA kwa kuanzisha hii ligi na mashindano
katika kata yetu. Mimi kama Polisi Kata nawaasa wananchi wote pamoja na vijana
kutumia fursa hii vizuri ili waweze kuibua vipaji vyao lakini pia kufikia
malengo yao waliyojiwekea katika michezo,” amesema Mashimba.
Amesema Jeshi la Polisi linaunga mkono mashindano hayo
kwa kuwa michezo imekuwa njia muhimu ya kuwafanya vijana kuwa bize na shughuli
zenye manufaa badala ya kukaa vijiweni na kujihusisha na matumizi ya dawa za
kulevya pamoja na vitendo vya kihalifu.
“Watu wanapokuwa kwenye michezo hawawezi
kuwaza mambo ya uhalifu kama uvunjaji, wizi na mambo mengine yasiyopendeza
katika jamii. Michezo ni afya, michezo ni urafiki, michezo ni ujamaa lakini pia
ni fursa kwa sababu watu wanatoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya mkoa
kukutana hapa,” ameongeza.
Aidha amewatahadharisha wananchi wenye nia ya kuvuruga
amani au kufanya vitendo vya kihalifu wakati wa mashindano hayo kuwa sheria
itachukua mkondo wake kwa yeyote atakayebainika kwenda kinyume na taratibu
zilizowekwa.
Mashimba amesema mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026
yanatambulika rasmi kuanzia ngazi ya serikali ya kijiji, serikali ya kata,
kamati ya ulinzi na usalama ya kata hadi ngazi ya wilaya pamoja na Baraza la
Michezo Mkoa wa Shinyanga hivyo mtu yeyote atakayevunja sheria atachukuliwa
hatua kali za kisheria ikiwemo kufikishwa polisi na mahakamani.
Mashindano hayo yameandaliwa na Paul Daud Augustino
kupitia ufadhili wa shirika la Lushu Foundation kwa lengo la kuibua vipaji vya
vijana, kuimarisha mshikamano wa jamii pamoja na kukuza michezo katika Mkoa wa
Shinyanga.
Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali,
matangazo pamoja na burudani unaweza kuwasiliana na Paul Daud Augustino kupitia
namba 0757 267 738.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment