Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania Mkoa wa
Katavi, Fortunata Kabeja, amefanya ziara katika kata 19 za Wilaya ya Mpanda
Aprili 5, 2026, akikutana na wanachama wa jumuiya hiyo pamoja na Chama Cha
Mapinduzi kwa lengo la kuimarisha uhai wa jumuiya na mshikamano.
Katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa CCM Wilaya
ya Mpanda, Kabeja aliwasalimia wanachama na kuwakumbusha umuhimu wa kuwa na
mawazo chanya ya kujenga jumuiya na chama kwa kushirikiana, kufanya mikutano ya
mara kwa mara na kupeana maelekezo ya kiutendaji.
Aidha, aliwashukuru wanachama kwa mchango wao mkubwa
uliopelekea ushindi wa chama katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 katika ngazi
mbalimbali, ikiwemo madiwani, wabunge na nafasi ya urais.
Akizungumzia uhai wa jumuiya, Kabeja aliwataka
wanachama kuongeza juhudi katika kulipa ada na kuandikisha wanachama wapya ili
kuimarisha jumuiya hiyo katika ngazi za mashina, matawi, kata na wilaya.
Katika hatua nyingine, aliahidi kutoa vyeti vya
shukrani kwa kata zitakazofanya vizuri kama njia ya kuhamasisha utendaji bora,
huku akisisitiza umuhimu wa umoja na mshikamano bila kubaguana.
Pia aliwataka wanachama kuendeleza upendo, amani na
kuheshimiana katika utekelezaji wa majukumu ya jumuiya na chama, akibainisha
kuwa maadili hayo ni msingi wa maendeleo na mafanikio ya pamoja.
Kabeja aliwahamasisha wanawake kujihusisha na shughuli
za ujasiriamali na kubuni miradi midogo midogo itakayowaongezea kipato,
sambamba na kuzingatia maadili ya nidhamu, uaminifu, uzalendo na ushirikiano.
Katika ziara hiyo, aliwataka viongozi wa ngazi
mbalimbali kuhakikisha wanakuwa na takwimu sahihi za wanachama, kufanya vikao
vya mara kwa mara, kutunza kumbukumbu, kusikiliza na kutatua kero za wanachama
kwa wakati.
Ziara hiyo ilihitimishwa kwa maelekezo kwa viongozi wa
mashina, matawi, kata na wilaya kuendelea kusimamia majukumu yao kwa
uwajibikaji, huku wakisisitizwa kubuni miradi ya maendeleo, kuimarisha
mawasiliano na kujenga mahusiano mazuri kati ya chama na serikali.
Ziara hiyo ilihusisha kata mbalimbali zikiwemo Kashaulili, Majengo, Misunkumilo, Nsemulwa, Kakese, Ibindi, Sitalike na Itenka, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha Jumuiya ya UWT na chama kwa ujumla katika Mkoa wa Katavi.
Ndg. Fortunata Kabeja, Mwenyekiti wa Jumuiya ya UWT Mkoa wa Katavi, akisaini kitabu cha wageni alipowasili Wilaya ya Mpanda.
Ndg. Taus, Mwenyekiti wa Jumuiya ya UWT Wilaya ya Mpanda, akiwasalimia na kuwakaribisha wajumbe kwenye kikao, kisha akakifungua na kuwaomba wajumbe kuwa na utulivu kumsikiliza Ndg. Fortunata Kabeja, Mwenyekiti wa Jumuiya ya UWT Mkoa wa Katavi.
Ndg. Mary, Katibu wa Jumuiya ya UWT Mkoa wa Katavi, akiwasalimia na kuwakaribisha wajumbe katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo mkoani Katavi.
Ndg. Jimotoli Jilala Maduka, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi, ambaye pia ni Kaimu Katibu wa Jumuiya ya UWT Wilaya ya Mpanda, ameshiriki kikamilifu katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Katavi, Ndg. Fortunata Kabeja, kilichofanyika katika Wilaya ya Mpanda.
Ndg. Jimotoli Jilala Maduka, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi, ambaye pia ni Kaimu Katibu wa Jumuiya ya UWT Wilaya ya Mpanda, ameshiriki kikamilifu katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Katavi, Ndg. Fortunata Kabeja, kilichofanyika katika Wilaya ya Mpanda.
Mh. Anna Joseph Mayaya, Diwani Viti Maalum wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda (Tarafa ya Misunkumilo) na Mjumbe wa Baraza Kuu la UWT Taifa, ameshiriki kikamilifu katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Katavi, Ndg. Fortunata Kabeja, kilichofanyika Wilaya ya Mpanda, akisisitiza umuhimu wa umoja na mshikamano pamoja na ubunifu wa miradi ya maendeleo kwa wanachama wa jumuiya.
Mh. Anna Joseph Mayaya, Diwani Viti Maalum wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda (Tarafa ya Misunkumilo) na Mjumbe wa Baraza Kuu la UWT Taifa, ameshiriki kikamilifu katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Katavi, Ndg. Fortunata Kabeja, kilichofanyika Wilaya ya Mpanda, akisisitiza umuhimu wa umoja na mshikamano pamoja na ubunifu wa miradi ya maendeleo kwa wanachama wa jumuiya.
Mh. Nuru Nkana, Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi, amewasalimia wajumbe katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Katavi, Ndg. Fortunata Kabeja, akisisitiza umuhimu wa umoja na mshikamano kwa pamoja ili kuhakikisha Jumuiya ya UWT inakuwa mstari wa mbele katika maendeleo na uongozi kwa ujumla.

Mh. Ashura, Diwani Viti Maalum wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda (Tarafa ya Kashaulili), ameshiriki kikamilifu katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Katavi, Ndg. Fortunata Kabeja, ambapo pia amewasalimia wajumbe wote katika kikao hicho.

Ndg. Munira Pesa Mbili, Mjumbe wa Kamati Ndogo ya Uchumi, Mipango na Fedha ya Jumuiya ya UWT Mkoa wa Katavi, amewasalimia na kuwashukuru wajumbe wote kwa kuhudhuria kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Katavi, Ndg. Fortunata Kabeja, kilichofanyika Wilaya ya Mpanda.
Pia ameshiriki kikamilifu katika kikao hicho, akisisitiza wanawake kuendelea kupambana na kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi zinazopatikana katika maeneo yao ili kuimarisha kipato na maendeleo ya familia na jamii kwa ujumla.
Wajumbe wa kikao hicho wameonekana wakiwa na utulivu mkubwa wakimsikiliza kwa makini Ndg. Fortunata Kabeja, Mwenyekiti wa Jumuiya ya UWT Mkoa wa Katavi, alipokuwa akitoa maelekezo na nasaha zake kuhusu uimarishaji wa jumuiya na mshikamano wa wanachama.
Wajumbe wa kikao hicho wameonekana wakiwa na utulivu mkubwa wakimsikiliza kwa makini Ndg. Fortunata Kabeja, Mwenyekiti wa Jumuiya ya UWT Mkoa wa Katavi, alipokuwa akitoa maelekezo na nasaha zake kuhusu uimarishaji wa jumuiya na mshikamano wa wanachama.
Ndg. Mary, Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Mkoa wa Katavi, ameshiriki kikamilifu katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Katavi, Ndg. Fortunata Kabeja, kilichofanyika Wilaya ya Mpanda, akisisitiza umuhimu wa upendo na amani ndani ya jumuiya na jamii kwa ujumla.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254











Post a Comment