Na Mapuli Kitina Misalaba
Ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 imeanza rasmi Mei 16, 2026
katika uwanja wa Mwabenda uliopo kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya
Shinyanga huku ikihusisha jumla ya timu 22 kutoka maeneo mbalimbali ndani na
nje ya Mkoa wa Shinyanga.
Mashindano hayo yamezikutanisha timu kutoka Mkoa wa
Mwanza, Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Geita, Manispaa ya Shinyanga pamoja na timu
kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambayo ndiyo jimbo la Solwa.
Mchezo wa ufunguzi ulikuwa kati ya HOME BOYS dhidi ya
MANHEIGANA ambapo timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 katika mchezo uliovutia
mashabiki ambao waliojitokeza kushuhudia uzinduzi wa mashindano hayo.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa na Katibu wa Kamati
ya Mashindano Sambayi Jilya, mchezo unaofuata utawakutanisha Wafukunyungu FC
kutoka Manispaa ya Shinyanga dhidi ya Mwasenge kutoka Halmashauri ya Wilaya ya
Shinyanga jimbo la Solwa.
Akizungumza katika uzinduzi wa mashindano hayo, mgeni
rasmi ambaye ni Diwani wa kata ya Solwa Mhe. Dotto Samson amempongeza mwandaaji
wa NIACHEKONA CUP 2026 kwa juhudi kubwa anazoendelea kuzifanya katika kuinua
vipaji vya vijana kupitia michezo.
“Nikupongeze sana Niachekona, uthubutu ni
jambo jema na hadi sasa dalili zilizopo umefaulu. Mwanzo huwa ni mgumu lakini
kwa sasa jina lako limeendelea kuwa maarufu na liendelee kuwa maarufu kwa
kuinua vipaji vya hawa vijana,” amesema Dotto Samson.
Aidha amesema anatamani mashindano hayo yawe chachu ya
mafanikio kwa vijana wanaopenda mpira wa miguu huku akisisitiza kuwa michezo ni
afya, ajira, burudani lakini pia ni biashara.
“Fanyeni kazi kwa malengo na muwe na
nidhamu. Unapokuwa ndani ya uwanja hakikisha amani inakuwepo kwako na kwa
mwenzako pia. Niwaombe mashabiki muendelee kuwa watulivu mnapokuwa uwanjani,”
ameongeza.
Kwa upande wake mwandaaji wa mashindano hayo Bwana
Paul Daud maarufu MC NIACHEKONA amesema kuwa huu ni msimu wa tatu wa mashindano
hayo kufanyika katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa.
“Hii ni awamu ya tatu kuandaa michuano hii
hapa Mwabenda. Lengo kubwa ni kuwasaidia vijana kuachana na matukio yasiyo na
maana na kuwaunganisha pamoja kupitia michezo huku wakielewa maana ya maisha na
umuhimu wa amani,” amesema MC NIACHEKONA.
Ameongeza kuwa watu wengi humuita “Azam Mdogo” au
“Jambo Mdogo” kutokana na namna anavyotumia nguvu na gharama kubwa kuhakikisha
mashindano yanaendeshwa kwa ubora mkubwa ikiwemo maandalizi ya timu, usafiri
pamoja na zawadi mbalimbali.
“Mimi kama mdau mkubwa wa michezo katika
eneo hili ninaomba wadau mbalimbali ikiwemo Azam, Jambo FM na wengine waweze
kunisapoti ili soka hili liendelee kukua na kusafiri salama,”
amesema.
Pia amewashukuru wafadhili wake mbalimbali
waliofanikisha kufanyika kwa mashindano hayo ya mwaka 2026 akiwemo Jambo FM
kupitia kipindi cha Extra Time pamoja na Mabula Lushulwanhambi wa Mahembe
ambaye amechangia maendeleo ya uwanja huo.
Mbali na michezo, MC NIACHEKONA ni Meneja wa Kishushu
Hotel na pia ni mchimba madini katika mgodi wa Mwakitolyo. Kwa huduma za MC
NIACHEKONA wasiliana naye kupitia namba 0757 267 738.
Kwa upande mwingine Polisi wa kata ya Solwa amewahakikishia
wananchi usalama wa kutosha katika kipindi chote cha mashindano hayo.
RATIBA YA MECHI – NIACHEKONA CUP 2026
Mei 16, 2026
HOME BOYS Vs MANHEIGANA
Mei 17, 2026
WAFUKUNYUNGU FC Vs MWASENGE
Mei 18, 2026
DUARA FC Vs MWANDUTU
Mei 19, 2026
SHILIMA Vs SONGAMBELE MHANGU
Mei 20, 2026
NYUNDO FC Vs NZOZA
Mei 21, 2026
MAHEMBE Vs MAWEMIRU
Mei 22, 2026
NYANDOLWA Vs BAJAJ FC
Mei 23, 2026
SHILABELA Vs LYABUKANDE
Mei 24, 2026
KIMANDAGULI Vs KASHISHI
Mei 25, 2026
ISENENGEJA Vs MWAKITOLYO No.6
Mei 26, 2026
SANGU FC Vs BULIGE
Viongozi wakisalimiana na wachezaji kabla ya kuanza kwa mchezo wa NIACHEKONA CUP 2026.
Mwandaaji wa mashindano hayo Bwana Paul Daud maarufu
MC NIACHEKONA akizungumza mbele ya mashabiki waliojitokeza katika uzinduzi wa
mashindano hayo.

Mwandaaji wa mashindano hayo Bwana Paul Daud maarufu
MC NIACHEKONA akizungumza mbele ya mashabiki waliojitokeza katika uzinduzi wa
mashindano hayo.
Katibu wa kamati ya mashindano Sambayi Jilya akisoma rasmi ratiba ya mechi za NIACHEKONA CUP 2026 mbele ya washiriki na mashabiki.
Polisi kata wa kata ya Solwa Paul Mashimba akiwahakikishia wananchi ulinzi na usalama kwenye ligi ya Niachekona 2026.
Kwa taarifa zote, matokeo ya mechi, ratiba pamoja na matukio mbalimbali ya NIACHEKONA CUP 2026, endelea kufuatilia Misalaba Media kupitia kurasa zake zote za mitandao ya kijamii.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

































































Post a Comment