
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mhe. Anord Makombe akizungumza na wananchi wakati wa maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM yaliyofanyika katika Kijiji cha Galamba, Kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga.Na Mapuli Kitina Misalaba
Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya
ya Shinyanga Mjini imeadhimisha miaka 71 tangu kuanzishwa kwa jumuiya hiyo,
huku viongozi wakitoa wito wa kuendelea kulinda maadili ya jamii, kuimarisha
malezi ya watoto na kudumisha amani ya Taifa.
Maadhimisho hayo yamefanyika katika Kijiji cha
Galamba, Kata ya Kolandoto katika Manispaa ya Shinyanga, ambapo mgeni rasmi ni Mwenyekiti
wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhe. Anord Makombe.
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mhe. Makombe
amesema Jumuiya ya Wazazi ina nafasi kubwa katika jamii kutokana na jukumu lake
la kusimamia malezi na maadili ya vijana, hasa katika kipindi hiki ambacho
kumekuwa na changamoto ya mmomonyoko wa maadili.
Amesema jamii inapaswa kushirikiana kwa pamoja na
taasisi mbalimbali kuhakikisha watoto wa kiume na wa kike wanapatiwa ulinzi na
mazingira bora yatakayowasaidia kutimiza ndoto zao kupitia elimu na maadili
mema.
“Jumuiya ya wazazi leo inaadhimisha miaka
71 kiwilaya na maadhimisho haya yanafanyika hapa Galamba. Jumuiya hii ina
majukumu mengi ikiwemo kushughulikia malezi ya vijana. Leo tunashuhudia
mmomonyoko wa maadili katika jamii, hivyo tunatakiwa kushirikiana kuhakikisha
watoto wetu wanapata malezi bora, elimu na kutimiza ndoto zao,”
amesema Makombe.
Aidha, Magombe amewataka wananchi kuendelea kudumisha
umoja, mshikamano na upendo huku wakimuomba Mungu katika maisha yao ya kila
siku, akieleza kuwa hali hiyo itasaidia kupunguza vitendo vya ukatili dhidi ya
watoto vinavyoendelea kujitokeza katika baadhi ya maeneo.
“Tuendelee kuwa wamoja na kushikamana ili
watu waendelee kuishi katika amani na upendo. Watu wakimuogopa Mungu itakuwa
vigumu kufanya vitendo vya ukatili dhidi ya watoto. Leo tunaona hata baadhi ya
wazazi wanawafanyia watoto wao ukatili, hivyo jamii inapaswa kusimama pamoja
kupinga hali hiyo,” ameongeza.
Katika hatua nyingine, Mhe. Makombe amesisitiza
umuhimu wa kulinda amani ya Tanzania, akiwataka wananchi kuwa wazalendo na
kutoa taarifa mapema pale wanapoona viashiria vinavyoweza kuhatarisha utulivu
wa nchi.
Amesema amani iliyopo nchini ni urithi mkubwa
ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere na kuendelezwa na viongozi
waliomfuatia, hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kuilinda.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko, amesisitiza umuhimu wa umoja na
mshikamano miongoni mwa wanajumuiya pamoja na wananchi kwa ujumla ili kuendelea
kujenga jamii yenye maadili na ustawi.
Naye Katibu wa Jumuiya hiyo wilayani humo, Bi. Doris
Kibabi, amesema katika kuadhimisha miaka 71 ya jumuiya hiyo wamefanikiwa
kutekeleza shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kutoa misaada kwa watu wenye
uhitaji pamoja na wagonjwa waliolazwa hospitalini.
Amesema pia jumuiya hiyo imepanda miti zaidi ya 361
ikiwa ni sehemu ya kampeni ya utunzaji wa mazingira na kuhamasisha wananchi
kushiriki katika uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti katika maeneo
mbalimbali.
Katika maadhimisho hayo, Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya
ya Shinyanga Mjini imetoa vyeti vya pongezi kwa taasisi na idara mbalimbali
zilizofanya vizuri katika utoaji wa huduma kwa jamii.
Miongoni mwa waliotunukiwa vyeti hivyo ni Idara ya Mazingira ya Manispaa ya Shinyanga kwa kuendelea kuwa kinara wa usafi kitaifa, Idara ya Elimu, Idara ya Ustawi wa Jamii pamoja na Jumuiya ya kupinga ukatili ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) kwa mchango wao katika kupambana na vitendo vya ukatili katika jamii.
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha akizungumza.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi. Doris Kibabi akieleza shughuli zilizotekelezwa na jumuiya hiyo ikiwemo utoaji wa misaada na upandaji wa miti zaidi ya 361 kwa ajili ya utunzaji wa mazingira.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mhe. Anord Makombe akizungumza wakati wa maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM yaliyofanyika katika Kijiji cha Galamba, Kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga.
Wananchi na wanachama wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini wakifuatilia kwa makini hotuba mbalimbali wakati wa maadhimisho ya miaka 71 ya jumuiya hiyo yaliyofanyika Kijiji cha Galamba Kata ya Kolandoto.
Wananchi na wanachama wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini wakifuatilia kwa makini hotuba mbalimbali wakati wa maadhimisho ya miaka 71 ya jumuiya hiyo yaliyofanyika Kijiji cha Galamba Kata ya Kolandoto.
Baadhi ya wananchi pamoja na wanachama wa Jumuiya ya Wazazi wakishiriki maadhimisho ya miaka 71 ya jumuiya hiyo huku wakihamasishwa kudumisha amani, umoja na malezi bora ya watoto.
Wanachama wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini wakiwa katika mkutano wa maadhimisho ya miaka 71 ya jumuiya hiyo uliofanyika Galamba Manispaa ya Shinyanga.
Wananchi wa Kijiji cha Galamba wakiwa katika maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM yaliyolenga kuhamasisha maadili, mshikamano na mapambano dhidi ya ukatili kwa watoto.
Wanachama na wananchi mbalimbali wakionesha ushirikiano na mshikamano wakati wa maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini.
Sehemu ya wananchi na wanajumuiya waliojitokeza kushiriki maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi yaliyofanyika katika Kijiji cha Galamba Kata ya Kolandoto.
Wananchi wa Kijiji cha Galamba wakiwa katika maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM yaliyolenga kuhamasisha maadili, mshikamano na mapambano dhidi ya ukatili kwa watoto.
Wananchi wa Kijiji cha Galamba wakiwa katika maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM yaliyolenga kuhamasisha maadili, mshikamano na mapambano dhidi ya ukatili kwa watoto.
Wananchi wa Kijiji cha Galamba wakiwa katika maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM yaliyolenga kuhamasisha maadili, mshikamano na mapambano dhidi ya ukatili kwa watoto.MR. BLACK
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mzee Fue Mrindoko akisisitiza umuhimu wa umoja na mshikamano kwa wanajumuiya pamoja na wananchi wakati wa maadhimisho ya miaka 71 ya jumuiya hiyo.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi. Doris Kibabi akieleza shughuli zilizotekelezwa na jumuiya hiyo ikiwemo utoaji wa misaada na upandaji wa miti zaidi ya 361 kwa ajili ya utunzaji wa mazingira.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi. Doris Kibabi akieleza shughuli zilizotekelezwa na jumuiya hiyo ikiwemo utoaji wa misaada na upandaji wa miti zaidi ya 361 kwa ajili ya utunzaji wa mazingira.
Diwani wa kata ya Kolandoto Mhe. Moses Mshagatila akieleza maendeleo na changamoto zinazowakabili wananchi wa kata yake.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi. Doris Kibabi akieleza shughuli zilizotekelezwa na jumuiya hiyo ikiwemo utoaji wa misaada na upandaji wa miti zaidi ya 361 kwa ajili ya utunzaji wa mazingira.
Mwenyekiti wa SMAUJATA Manispaa ya Shinyanga, Meryester Nyarusanda, akitoa elimu ya masuala ya ukatili kwenye maadhimisho ya Miaka 71 ya Jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mhe. Anord Makombe akizungumza na wananchi wakati wa maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM yaliyofanyika katika Kijiji cha Galamba, Kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa ya Shinyanga, Mwl. Richard Makoye akipokea cheti cha idara ya elimu.
Mkuu wa idara ya Maliasili na Mazingira Manispaa ya Shinyanga Mwl. Ezra Manjerenga akipokea cheti cha idara yake.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Bi. Doris Kibabi akipokea zawadi ya pongezi wakati wa maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi yaliyofanyika Kijiji cha Galamba, Kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Bi. Doris Kibabi akimshukuru Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mzee Fue Mrindoko.

Picha yao ya pamoja. Katibu na Mwenyekiti.
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha akipanda mti.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akishiriki zoezi la upandaji miti lililoandaliwa katika maadhimisho ya miaka 71 ya Jumuiya ya Wazazi yaliyofanyika Galamba.
Mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya Jumuiya ya wazazi Bi. Husna Maige akipanda mti.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254























































Post a Comment