" VITA YA NUSU FAINALI LEO: UFUKUNYUNGU FC NA DUARA FC KUPIGANIA FAINALI

VITA YA NUSU FAINALI LEO: UFUKUNYUNGU FC NA DUARA FC KUPIGANIA FAINALI


Na Mapuli Kitina Misalaba

Macho na masikio ya mashabiki wa soka leo Juni 18, 2026 yataelekezwa katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, ambapo Ufukunyungu FC na Duara FC zitamenyana katika mchezo wa nusu fainali unaotarajiwa kuamua timu ya kwanza kufuzu fainali ya NIACHEKONA CUP 2026.

Timu hizo mbili zimeonyesha kiwango kizuri tangu kuanza kwa mashindano hayo na leo zinakutana katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku kila upande ukiwa na ndoto ya kutinga fainali.

Mashabiki wa timu zote mbili wameendelea kutoa kauli za kujiamini kuelekea mchezo huo, hali inayoongeza hamasa na mvuto wa pambano hilo ambalo linatarajiwa kuvuta idadi kubwa ya watazamaji.

Wakati huo huo, mchezo wa pili wa nusu fainali utachezwa kesho, Ijumaa Juni 19, 2026, ambapo Bulige FC itamenyana na Kashishi FC kusaka tiketi ya pili ya kucheza fainali ya NIACHEKONA CUP 2026.

Mashindano hayo yameandaliwa na Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu Foundation, yakilenga kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo na kuimarisha mshikamano wa jamii.

Kwa huduma za MC, matangazo na ushereheshaji wa matukio mbalimbali, wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post