" NIACHEKONA CUP 2026 YAENDELEA KUPAMBA MOTO, DUARA FC YAITWANGA MWANDUTU 3-0

NIACHEKONA CUP 2026 YAENDELEA KUPAMBA MOTO, DUARA FC YAITWANGA MWANDUTU 3-0


Na Mapuli Kitina Misalaba

Ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 inayoendelea katika uwanja wa Kijiji cha Mwabenda kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga imeendelea kupamba moto ambapo timu ya DUARA FC imeibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya MWANDUTU katika mchezo uliochezwa leo Mei 18, 2026.

Mashindano hayo yaliyoanza rasmi Mei 16, 2026 yanashirikisha jumla ya timu 22 kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Shinyanga ikiwemo Mwanza, Geita, Kahama, Manispaa ya Shinyanga pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga jimbo la Solwa.

Katibu wa Kamati ya Mashindano Sambayi Jilya amesema michezo ya NIACHEKONA CUP 2026 itaendelea kesho ambapo timu ya SHILIMA kutoka Mwanza itashuka dimbani kuivaa SONGAMBELE MHANGU katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na ubora wa timu hizo.

Naye mwandaaji wa mashindano hayo Bwana Paul Daud maarufu MC NIACHEKONA amesema mafanikio ya mashindano hayo yanatokana na ushirikiano mkubwa kutoka kwa wananchi, wadau wa michezo pamoja na timu zinazoshiriki ambazo zimeonesha nidhamu na ushindani wa hali ya juu tangu kuanza kwa ligi hiyo.

Amesema dhamira yake ni kuona vijana wa Solwa na maeneo mengine wanapata jukwaa la kuonesha uwezo wao wa kisoka huku mashindano hayo yakizidi kuwa sehemu ya kuimarisha mshikamano, burudani na kuibua vipaji vitakavyoweza kufika katika ngazi kubwa za soka nchini.

MC NIACHEKONA pia amewashukuru wadhamini na marafiki mbalimbali wanaoendelea kuunga mkono mashindano hayo huku akisema mchango wao umeendelea kusaidia kukuza michezo katika kata ya Solwa na maeneo jirani.

Amewataja baadhi ya wadau wanaoendelea kutoa ushirikiano kuwa ni pamoja na Jambo FM kupitia kipindi cha Extra Time pamoja na Mabula Lushulwanhambi wa Mahembe kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha maendeleo ya michezo na uwanja wa Mwabenda.

Mbali na kuwa mwandaaji wa NIACHEKONA CUP 2026, Bwana Paul Daud maarufu MC NIACHEKONA pia ni Meneja wa Kishushu Hotel na mchimba madini katika mgodi wa Mwakitolyo. Kwa huduma za ushereheshaji (MC), matangazo na shughuli mbalimbali wasiliana naye kupitia namba 0757 267 738.

Viongozi mbalimbali pamoja na wadau wa michezo wakifuatilia mchezo wa NIACHEKONA CUP 2026 katika uwanja uliopo Mwabenda kata ya Solwa.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




 

Post a Comment

Previous Post Next Post