" SHUWASA YATAMBUA MCHANGO WA VYOMBO VYA HABARI KATIKA MAENDELEO

SHUWASA YATAMBUA MCHANGO WA VYOMBO VYA HABARI KATIKA MAENDELEO

Na Mapuli Kitina Misalaba

Katika maadhimisho ya World Press Freedom Day, Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) imetambua mchango mkubwa wa vyombo vya habari katika kuhabarisha, kuelimisha na kuchochea maendeleo ya jamii.

Akizungumza kwa niaba ya taasisi hiyo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa SHUWASA Bwana Jonas Mush amesema kuwa vyombo vya habari ni wadau muhimu ambao wamekuwa wakishirikiana kwa karibu na mamlaka hiyo katika utekelezaji wa majukumu yake kwa muda mrefu.

Amesema kupitia vyombo vya habari, SHUWASA imekuwa ikifikisha ujumbe kwa wananchi kwa urahisi zaidi, ikiwemo kutoa elimu kuhusu huduma za maji na usafi wa mazingira pamoja na kuwahabarisha kuhusu shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na taasisi hiyo.

Aidha, ametoa wito kwa taasisi nyingine kuonyesha ushirikiano kwa waandishi wa habari, hasa wanapohitaji taarifa au wanapowasilisha changamoto za wananchi, ili kusaidia kuboresha utoaji wa huduma kwa jamii.

Ameongeza kuwa uhuru wa vyombo vya habari ni kichocheo cha maendeleo, akisisitiza kuwa taasisi zinazotoa nafasi kwa waandishi kufanya kazi zao kwa uhuru hupata fursa ya kutambua na kutatua changamoto zinazojitokeza kupitia taarifa zinazoripotiwa.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post