" VIJANA WATAKIWA KUJISHUGHULISHA ILI KUJENGA TAIFA ENDELEVU

VIJANA WATAKIWA KUJISHUGHULISHA ILI KUJENGA TAIFA ENDELEVU

 Na Edington Mukiza Ezron, Misalaba Media

Baadhi ya wananchi katika Manispaa ya Shinyanga wamewataka vijana kuwajibika na kujishughulisha ili kuepukana na umasikini na kuliimarisha taifa kiuchumi.

Wameyasema hayo leo Mei,26,2026 kwa nyakati tofauti walipotembelewa na Misalaba Media.

Akizungumza mmoja wa wananchi hao Dickson Christopher amesema kuwa vijana wanatakiwa kupambana kujishughulisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kujitengenezea maisha mazuri kwa sasa na badae kwani vijana ndiyo nguzo ya jamii na taifa kwa ujumla.

Ameongeza kuwa vijana wanapofanya kazi za kuwaingizia kipato husaidia katika kuimarisha uchumi wa jamii na wa taifa kwani huongeza kiwango cha ulipaji Kodi hata uwekezaji nchini jambo ambalo linainua uchumi kwa kiasi kikubwa.

Naye David John amesema kuwa baadhi ya vijana wanashindwa kuwa wabunifu na kuwa na malengo jambo ambalo linawapelekea kukosa kazi za kufanya na kufanya uharifu licha ya kuwepo fursa mbalimbali za kiuchumi.

Pia amesema kuwa vijana wanatakiwa kupata mafunzo ya ufundi na fani mbalimbali za kujiajiri kutokana na hali ya ukosefu wa ajira kuliko kukaa mtaani bila kazi za kufanya ni muhimu wakawa na ujuzi juu ya fani mbalimbali.

Wananchi hao wameendelea kusema kuwa vijana wanatakiwa kuwa na maadili, nidhamu na kuepuka matendo yasiyofaa ili kuweza kufanikiwa katika kazi zao wanazozifanya kwani nidhamu ndio misingi wa mafanikio.

Aidha wameiomba serikali kutoa fursa mbalimbali kwa vijana ili kuwawezesha kiuchumi na kuboresha maisha yao na taifa ikiwemo kutoa mikopo yenye riba nafuu na kutoa ajira kwa wingi katika kampuni na taasisi mbalimbali.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

 

Post a Comment

Previous Post Next Post