Na Mapuli Kitina Misalaba
Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Shinyanga,
Johnson Japheth Chinyong'ole, amewataka Watanzania kuendelea kuilinda na
kuitunza amani ya nchi kwa kujiepusha na vitendo vinavyoweza kusababisha
migogoro, chuki na mifarakano katika jamii.
Askofu Chinyong'ole ametoa wito huo wakati wa ibada
maalum ya kumstaafisha Mchungaji Kanoni Jackson Daudi Iseke baada ya
kulitumikia Kanisa kwa miaka mingi, na kwamba imefanyika katika Kanisa la
Anglikana Solwa Kashishi, akisisitiza kuwa amani ni msingi muhimu wa maendeleo
ya taifa na ustawi wa wananchi.
Amesema kuwa bila amani hakuna maendeleo yanayoweza
kupatikana, hivyo kila mwananchi ana wajibu wa kuhakikisha anashiriki katika
kuijenga na kuilinda amani iliyopo nchini.
Aidha, amewahimiza viongozi wa dini na wananchi
kutumia maneno ya upendo, hekima na maridhiano katika kushughulikia tofauti za
mawazo ili kudumisha mshikamano miongoni mwa Watanzania.
Baadhi ya waumini waliohudhuria ibada hiyo akiwemo James
Nangi, Elizabeth Jackson, Paul Yohana na Eliana Charles wameeleza umuhimu wa
kuendelea kuombea taifa na viongozi wake, wakisema kuwa amani iliyopo nchini
imewezesha wananchi kufanya shughuli zao za maendeleo kwa utulivu.
Wamesema kuwa jamii inapaswa kuendelea kuhubiri
upendo, umoja na mshikamano ili kuimarisha amani iliyojengwa kwa miaka mingi
nchini Tanzania.
Waumini hao wamewataka vijana kujiepusha na vitendo
vya vurugu na badala yake kujikita katika shughuli za uzalishaji mali na
maendeleo ya taifa, huku wakisisitiza kuwa amani ni nguzo muhimu ya maendeleo
endelevu.
Wamesema kuwa ushirikiano kati ya viongozi wa dini,
Serikali na wananchi ni muhimu katika kuendelea kuimarisha umoja wa kitaifa na
kudumisha sifa ya Tanzania kuwa kisiwa cha amani barani Afrika.
Askofu Johnson Japheth Chinyong'ole akitoa mahubiri na nasaha mbalimbaliSHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




Post a Comment